Simba waijia juu Yanga sakata la Okwi
HomeMichezoKitaifa

Simba waijia juu Yanga sakata la Okwi

MSHAMBULIAJI wa Simba, Mganda, Emmanuel Okwi, ameibuka na kudai hana muda wa kuumiza kichwa juu ya madai ya klabu yaYanga, huku Mwenyeki...

Urais 2015: Ukawa waanza safari
Niyonzima aitwa timu ya Taifa
Serikali sasa yaalika wawekezaji wa Ghuba


MSHAMBULIAJI wa Simba, Mganda, Emmanuel Okwi, ameibuka na kudai hana muda wa kuumiza kichwa juu ya madai ya klabu yaYanga, huku Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya timu hiyo, Zacharia Hanspope akiwapa onyo kuwa endapo watafungua kesi wahakikishe wana vielelezo sahihi.

Yanga ilitangaza kumfungulia kesi ya madai ya fidia Okwi, kwa kumtaka ailipe kiasi cha dola 2,100,000 kwa kuvunja mkataba na ada ya mazoezi, huku ikidai kulipeleka suala hilo Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) ili liweze kupatiwa ufumbuzi.
Akizungumza na MTANZANIA akiwa visiwani Zanzibar, Okwi alisema hana tatizo na klabu yake hiyo ya zamani hivyo kama wapo tayari kwenda mahakamani ni vyema wakafanya hivyo ili sheria ziweze kufuatwa.

Alisema kwa sasa anataka kutuliza akili yake kufikiria masuala ya soka kwa kushirikiana na wenzake ili kufikia malengo yake na kwamba madai ya Yanga hayamuhusu, kwani amejipanga na tayari ameandaa watu watakaofuatilia suala hilo.

“Kwa sasa akili yangu inawaza mambo ya soka kwani nilikuja Tanzania kucheza mpira hivyo masuala yaYanga hayanihusu, kama wanataka kwenda mahakamani waende ila watambue sheria pekee ndio itatoa haki juu ya hilo,” alisema.
Kwa upande wake Hanspope, aliionya Yanga juu ya uamuzi wao wa kutaka kwenda mahakamani kumshtaki Okwi, huku akiwataka kuhakikisha kuwa na vielelezo vyote.

“Yanga wanatakiwa kuwa makini na jambo hili kwani asilimia kubwa wao ndio wenye matatizo, lakini kama wanataka kwenda mahakamani waende ila wanapaswa kuwa na vielelezo sahihi vinginevyo kesi hiyo itawageukia,” alisema.
Alisema lengo la uongozi wa Yanga ni kutaka kumchanganya kisaikolojia Okwi na kumtoa mchezoni ili ashindwe kuitumikia vyema Simba na kuwatahadharisha endapo wataenda mahakamani, watambue watakutana na majibu kama yaliyotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ya kumuidhinisha kuichezea klabu hiyo.

Share na rafiki yako hapo chini
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Simba waijia juu Yanga sakata la Okwi
Simba waijia juu Yanga sakata la Okwi
http://mtanzania.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/okwii-300x216.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/simba-waijia-juu-yanga-sakata-la-okwi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/simba-waijia-juu-yanga-sakata-la-okwi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy