MADAI YA KUBEBA UNGA: RAY C AJISALIMISHA POLISI
HomeMatukio

MADAI YA KUBEBA UNGA: RAY C AJISALIMISHA POLISI

Stori Na Musa Mateja/Ijumaa Wikienda   BAADA ya kukiri kwa mdomo wake kutumia madawa ya kulevya ‘unga’ na baadaye ‘kustaafu’, madawa hay...



Stori Na Musa Mateja/Ijumaa Wikienda
 
BAADA ya kukiri kwa mdomo wake kutumia madawa ya kulevya ‘unga’ na baadaye ‘kustaafu’, madawa hayohayo yamemletea msanii Rehema Chalamila ‘Ray C’ ‘msala’ ambao umemfanya yeye mwenyewe, kwa hiyari yake ajisalimishe polisi.

Msanii wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ akiwa Hospitali ya Mwananyamala .

Hivi karibuni, Ray C alijikuta akiangua kilio ndani ya Kituo cha Polisi cha Kijitonyama ‘Mabatini’, Dar baada ya kuhusishwa na ishu ya uuzaji wa unga.

KAWE DARAJANI
Chanzo hicho kilinyetisha kwamba, siku ya tukio, wakati Ray C akitokea nyumbani kwake, alipofika maeneo ya Kawe Darajani aliona pikipiki ikimfukuzia na baadaye ikampita na ‘kumbloku’.
Ilisemekana kwamba baada ya kusimama, jamaa alishuka kwenye pikipiki kisha akamwambia aegeshe pembeni gari lake aina ya Toyota Carina TI.

Chanzo kilidai kwamba, Ray C alikataa kufanya hivyo kwa kuhisi aliyekuwa akimwamrisha ni jambazi.
“Ray C aliamua kuondoa gari kwa kulazimisha ambapo alimkwepa jamaa huyo kisha kukanyaga mafuta ambapo gari liliondoka kwa kasi,” alisema.

LUGALO
Ilisemekana kwamba baada ya kufika kwenye kituo cha daladala cha Lugalo, alisimama na jamaa huyo aliyekuwa akimfukuzia akaegesha pikipiki mbele yake na kumtaka Ray C ashuke ndani ya gari kwani alitaka kulipekua akimwambia kuwa alikuwa amebeba unga.
Ishu hiyo ilizidi kumtia Ray C wasiwasi na kumuuliza jamaa huyo ni nani ambapo alisema kuwa yeye ni askari.
Kwa kuwa hakuwa na sare, Ray C hakuamini jambo lililosababisha jamaa huyo kumuonesha kitambulisho kilichokuwa kimechakaa.

‘Ray C’akiingia kwenye gari lake aina ya 'Toyota Carina'.

MAELEWANO YASHINDIKANA
Baada ya kuona hivyo, Ray C alimwambia waongozane hadi Kituo cha Polisi cha Oysterbay lakini jamaa huyo alikataa na kumtaka waende Kawe jambo ambalo Ray C alishindwa kuafikiana nalo na kuondoa gari lake akimwambia waambatane hadi Kituo Kidogo cha Polisi cha Mwenge.

Jamaa huyo alionekana kutotaka kwenda hivyo Ray C aliondoa gari kwa kasi na kuelekea Mwenge ambako alikuwa akiomba msaada kwa matrafiki na alipoona wanachelewa aliondoa gari kumkimbia jamaa huyo.
Ilisemekana kwamba awali alitaka kukimbilia Kituo cha Polisi cha Mwenge lakini alipoona kuna msongamano alikimbia kwenda kujisalimisha Mabatini huku akiangua kilio.

BOFYA HAPA KUMSIKIA RAY C
Baada ya kushibishwa taarifa hiyo, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Ray C ambaye alielezea mkasa mzima.
Alifunguka: “Ni kweli ulivyoambiwa tulitoka Lugalo na kuelekea Mwenge baada ya kufika kwenye makutano ya Mwenge niliwaona askari wawili na trafiki akiwa pembeni, nikawasimamisha na kuwaeleza.
“Askari mmoja alikubali kupanda kwenye gari langu nikaenda naye hadi Mabatini.

“Baada ya kufika Mabatini nilieleza kila kitu kwa mkuu wa kituo hivyo akaniambia nisiwe na wasiwasi.
“Bada ya hapo mkuu wa kituo aliita askari wa kike na wa kiume nikaongozana nao hadi katika gari langu na kupekua kila sehemu lakini wakasema hapakuwa na chochote kibovu, hivyo nikawa nalia tu na mkuu wa kituo akaniomba ninyamaze na kuniruhusu nikaondoka zangu kwenda Hospitali ya Mwananyamala kumeza dawa.
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: MADAI YA KUBEBA UNGA: RAY C AJISALIMISHA POLISI
MADAI YA KUBEBA UNGA: RAY C AJISALIMISHA POLISI
http://api.ning.com/files/FkLMylrJqnVvgbjB9CsruVh-KDufv1lBG9rYylQElyW5tyZIY7S-SVKMSFcXTWxK3V*kGI6B03X-iHLHOdRSBTdjd-VssJX-/2.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/madai-ya-kubeba-unga-ray-c-ajisalimisha.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/madai-ya-kubeba-unga-ray-c-ajisalimisha.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy