JOH MAKINI:MUZIKI UMENIFANYA NISIWE PAKA ROAD
HomeMuziki

JOH MAKINI:MUZIKI UMENIFANYA NISIWE PAKA ROAD

NI siku nyingine tena tunakutana katika Live Chumba cha Habari cha Global Publishers, na leo tunaye staa wa michano ya Hip ...

New Audio: Ben Pol – Sophia
New Audio: Diamond Platnumz – Nasema Nawee
Video Mpya: Cassim Mganga – Moto Moto


NI siku nyingine tena tunakutana katika Live Chumba cha Habari cha Global Publishers, na leo tunaye staa wa michano ya Hip Hop kutoka Arusha, John Simon ‘Joh Makini’ambaye alianza kufahamika kuanzia miaka ya 2004/2005 alipotoka na wimbo wake wa Hao, Hawapendi na Chochote, pia ni mmoja kati ya wasanii wanaounda Kundi la Weusi na ni memba wa River Camp Soldiers. 

Joh Makini akilonga na Global TV Online.

Katika mahojiano aliyoyafanya na Global TV Online hivi karibuni ambayo yataruka hewani kesho Jumatano katika kipindi cha Mtu Kati kupitia tovuti ya www.globaltvtz.comwww.globaltvtz.com Joh alifunguka;

Mwandishi: Unauzungumziaje muziki wa Hip Hop kwa ujumla?
 

Joh Makini: Muziki wa Hip Hop kwa Tanzania ndiyo muziki anzilishi kabla ya miziki yote hii inayosikika watu walikuwa wanarap baadaye ndiyo ikaja R&B ambayo haikuwa na soko, Bongo Fleva ilikuja kutokea baadaye, nimekuwa nikishiriki kwenye matamasha mengi na nimegundua wasanii wa Hip Hop wakipanda kwenye jukwaa kunakuwa na hali tofauti yaani muamko mkubwa tofauti na wasanii wengine.

Mwandishi: Kundi lenu la Weusi mpo watano lakini mara nyingi stejini mmekuwa mkionekana watatu yaani wewe, Nick wa II na G Nako ni kwa nini?Joh Makini: Tuko memba watano, mmoja ni daktari anafanya kazi Kahama anaitwa Bonta. Suala la Bonta kutokuwepo kwenye steji na kukosekana kwenye baadhi ya nyimbo za Kundi la Weusi hakuna tofauti yeyote tuko vizuri tu, Lord Eyez alikuwa amesimamishwa na ndiyo maana hakuonekana kwenye steji kwa mwaka jana lakini kwenye matamasha mawili ya kufungia mwaka na Weusi alionekana.

Mhariri wa Gazeti la Risasi Jumamosi, Erick Evarist (kushoto) akipozi na Joh Makini
.
Mwandishi: Unapata changamoto zipi kwa kufanya kazi na mdogo wako katika kundi moja?
Joh Makini: Kwenye undugu kuna wakati unakaa pembeni, kazi inachukua nafasi yake na kinachotuongoza ni Mwenyezi Mungu, Upendo na kuheshimiana, kizuri ni kwamba tulipokutana kila mtu alikuwa anajitegemea kwa maana kila mtu ana biashara zake  na tukifanya kazi ya kampuni tunakutana kama Weusi Kampuni na tunafanya. Nasikia faraja sana kuzaliwa na ‘Genious’ na kufanya kazi na Nick wa II ni baraka kwangu. 

Mwandishi: Nitajie wasanii watatu wa muziki wa Hip Hop ambao unawakubali sana hapa Bongo.
 

Joh Makini: Wapo wengi sana siwezi kuwataja na hata nje wapo wengi kama G2, Nas, 50 Cent,2 Pac, Notorious BIG na wengine kibao.
Mwandishi: Unawasaidia vipi wasanii chipukizi hasa kutoka Arusha ambako ndiyo chimbuko lenu na kuweza kujiunga na Kundi la Weusi?Joh Makini: Tunataka wasanii na siyo kila rapa ana uwezo wa kuungana na Weusi, milango yetu iko wazi siku zote na hata ukija pale River Camp wapo ambao bado tuko kwenye levo ya kuwapa ushauri lakini siyo kusema tutamchukua mtu na kumpeleka studio kwa sababu bado hajafikia ile levo ya michano ambayo sisi tupo. 

Martha Mboma (kulia), Omary Mdose (kushoto) wakipozi na Joh Makini.

Mwandishi: Unazungumziaje suala la wasanii kwenda kushuti video nje ya nchi? Mfano wasanii wengi kukimbilia nchini Afrika Kusini.Joh Makini: Suala la wasanii kwenda kufanya video nje ya nchi mimi nalisapoti kwa sababu siyo kitu kibaya kwa kuwa muziki hauna mipaka kwa hiyo watu wanapokwenda kufanya video Afrika Kusini au Nigeria wanafuata ubora na kikubwa ambacho kinawatoa wasanii wa Afrika Mashariki na wengine kufanya video kule ni wazi kwamba madairekta wa Afrika Kusini wana mawasiliano moja kwa moja na Trace TV, MTV na Channel O ambao wamekuwa wanasimamia na ndiyo maana inakuwa rahisi.
Mwandishi: Ni dairekta gani mbali na Nisher ambaye unamkubali na upo tayari kufanya naye kazi?

Joh Makini: Fundi Samweli  ambaye nimefanya naye ngoma moja tu redioni lakini bado nipo kwenye mchakato wa kufanya naye ngoma nyingine nyingi.

Kigogo wa Kitengo cha IT Global, Clarence Mulisa akipozi na Joh Makini.

Mwandishi: Mafanikio yapi umeyapata kupitia muziki?
Joh Makin: Muziki unaendesha maisha yangu, kijana kama mimi kwa akili nilizonazo kama ningezitumia tofauti nafikiri ningekuwa paka road. Namshukuru Mungu kwa kipaji nilichonacho, muziki umenikutanisha na watu wengi na kunipa heshima japo kuna vitu vingi ambavyo bado naudai.
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: JOH MAKINI:MUZIKI UMENIFANYA NISIWE PAKA ROAD
JOH MAKINI:MUZIKI UMENIFANYA NISIWE PAKA ROAD
http://api.ning.com/files/lET3ABatHUn-r1wWMLAn*-HKdZc6e3jkTcvUmWQEIWwYD49OqwlNwEH1iE-6iSnmVobvdnP0iwdeu**-fIwjUDfSf9YwiGfP/uwazii.77777777.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/joh-makinimuziki-umenifanya-nisiwe-paka.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/joh-makinimuziki-umenifanya-nisiwe-paka.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy