Jaji Warioba Dar es Salaam. Wakati Taifa zima likiwa katika kitendawili cha kumjua kiongozi wa nchi atakayepatikana baada ya Uchaguz...
Akizungumza katika mahojiano maalumu jana, Jaji
Warioba alisema si kazi ngumu kwa Watanzania kumfahamu rais ajaye kwa
kuwa katika miaka 50 tangu tupate uhuru, Watanzania wanazijua sifa za
kiongozi bora.
Jaji Warioba alisema; “Tatizo la kumjua rais afaaye tunalikwepa lakini linafahamika. Wanaotumia fedha na lugha chafu katika kampeni na hao ndiyo wasiotakiwa.”
“Katika miaka 50 tunazijua sifa za kiongozi bora.
Hapa tunakwepa tatizo tu. Tatizo ni matumizi ya fedha na lugha chafu
katika kampeni,” alisema Jaji Warioba ambaye pia ni waziri mkuu mstaafu.
Hadi sasa wanasiasa zaidi ya 20 wakiwamo wa CCM na
upinzani wamekuwa ama wanatajwa au wameonyesha nia ya kugombea nafasi
ya urais katika uchaguzi mkuu ujao.
Ukiacha wale wanaotajwa, wanasiasa waliotangaza nia hiyo kutoka CCM ni Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, Mbunge wa Nzega, Hamis Kigwangala na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, huku Mbunge wa Wawi (CUF), Hamad Rashid Mohamed akitangaza nia kupitia ADC.
Akifafanua zaidi, Jaji Warioba alisema kila mtu anaweweseka kuhusu kiongozi anayefaa ingawa ni kazi rahisi kumjua kutokana na ujuzi tulionao wa miaka zaidi ya 50 ya uhuru.
Kadhalika, Jaji Warioba alisema viongozi wa
Serikali hawana budi kuangalia taswira ya uchaguzi mkuu ujao kupitia
uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao umeonekana kuwa na kasoro
zilizosababisha vurugu.
“Nchi hii ina amani na tujitahidi kuilinda amani
yetu. Katika uchaguzi huu tufanye kila tuwezalo kuweka maandalizi yenye
umakini,” alisema Warioba na kuongeza: “Nasisitiza amani. Uchaguzi wa
Serikali za Mitaa ni funzo.”
Tetesi kuwania urais
Hivi karibuni baadhi ya vyombo vya habari, likiwamo gazeti la chama tawala, viliripoti tetesi kuwa Jaji Warioba anaandaliwa kuwania urais kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), tetesi ambazo kiongozi huyo alizikanusha vikali.
Jaji Warioba alisema amelitumikia Taifa kwa muda mrefu na aling’atuka kwa mapenzi yake, hivyo hawezi kurudi tena katika siasa.
“Hii ni Januari, kama watafuata sheria na kuanza kutoa elimu kwa kipindi cha miezi miwili, ina maana itakuwa ni Aprili na Mei, ukijumlisha mwezi mmoja wa kampeni ambao ni Juni ina maana kura itapigwa Julai. Ikumbukwe kuwa mwezi huo mbio za uchaguzi zitakuwa zimepamba moto,” alisema. Kura hiyo ya maoni imepangwa kufanyika Aprili 30.
Jaji Warioba alisema ni vyema kama mchakato wa Katiba mpya ukaenda kama sheria inavyosema kwani kinyume na hapo mambo yataharibika na pengine vurugu zinaweza kutokea katika uchaguzi mkuu.
“Nimetukanwa sana, nimebezwa, nimekejeliwa kwa mambo mengi
lakini ukweli ni kuwa nilifanya uamuzi wa kung’atuka katika siasa miaka
20 iliyopita na siwezi kubadili uamuzi wangu,” alisema.
Akizungumzia baadhi ya wanasiasa kutumia jina lake
katika majukwaa na baadhi kumkashifu kwa madai kuwa alimsaliti Baba wa
Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Jaji Warioba aliwataka wanaofanya hivyo
wasitumie jina lake kusafisha njia zao katika siasa.
“Nimeitumikia nchi hii kwa miaka 30, kuanzia mwaka
1966 hadi 1995 nikang’atuka. Niliufanya uamuzi huo miaka 20 iliyopita,
nikabaki katika uongozi wa chama nako nikaachia ngazi 2002. Mjue kuwa
nilifanya hayo kwa umakini mkubwa,” alisema.
Utata Kura ya Maoni
Katika mahojiano hayo, pia Jaji Warioba
alizungumzia mchakato wa kuboresha Daftari la Wapigakura na Sheria ya
Kura ya Maoni kuwa mwingiliano wake hasa katika kipindi cha uchaguzi
utaleta mkanganyiko.
Akizungumzia mkanganyiko huo, Jaji Warioba alisema
sheria inaweka utaratibu maalumu wa mchakato wa kura ya maoni ambao
alisema hautaendana na ratiba ya uandikishwaji katika daftari hilo.
“Kwa utaratibu uliowekwa, Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC) itamaliza kazi Machi na wakati huo kura ya maoni
imepangwa kufanyika Aprili. Kwa hali hiyo hatuna uhakika kama Tume
itakamilisha kazi yake katika kipindi hicho,” alisema.
Jaji Warioba alisema Sheria Kura ya Maoni Na. 3 ya
mwaka 2014 inasema kuwa wananchi wanatakiwa kupewa elimu ya kura ya
maoni kwa kipindi cha miezi miwili na mwezi mmoja wa kampeni lakini hadi
sasa hakuna ratiba inayoeleweka, jambo ambalo linaleta mwingiliano.
“Hii ni Januari, kama watafuata sheria na kuanza kutoa elimu kwa kipindi cha miezi miwili, ina maana itakuwa ni Aprili na Mei, ukijumlisha mwezi mmoja wa kampeni ambao ni Juni ina maana kura itapigwa Julai. Ikumbukwe kuwa mwezi huo mbio za uchaguzi zitakuwa zimepamba moto,” alisema. Kura hiyo ya maoni imepangwa kufanyika Aprili 30.
Jaji Warioba alisema ni vyema kama mchakato wa Katiba mpya ukaenda kama sheria inavyosema kwani kinyume na hapo mambo yataharibika na pengine vurugu zinaweza kutokea katika uchaguzi mkuu.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju hakupatikana kuzungumzia utata huo wa kisheria.
“Nilikwenda Malawi mwaka 2004 nikaona utaratibu wa BVR umeleta changamoto kwa sababu tu ni teknolojia mpya. Inahitajika elimu ya kina kabla ya matumizi yake,” alisema Jaji Warioba.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva alisema tume hiyo imeshazifanyia majaribio mashine hizo katika majimbo matatu na zimeonyesha ubora na upungufu ulikuwa mdogo huku zile zenye kasoro zikifanyiwa marekebisho.
Chanzo MWANANCHI
Kuhusu matumizi ya BVR
Kadhalika, Jaji Warioba alisema kwa matumizi ya
teknolojia BVR katika hatua ya maboresho ya daftari la kudumu la
wapigakura, kwa uzoefu alio nao, vifaa hivyo vina utata mkubwa hivyo
unahitajika umakini mkubwa.
“Nilikwenda Malawi mwaka 2004 nikaona utaratibu wa BVR umeleta changamoto kwa sababu tu ni teknolojia mpya. Inahitajika elimu ya kina kabla ya matumizi yake,” alisema Jaji Warioba.
Alitoa mfano wa utata wa BVR kuwa iwapo mpigakura
atafanya udanganyifu na kujiandikisha mara mbili au zaidi (hata kama
atatumia majina tofauti), mashine itafuta majina yaliyozidi na kubaki na
taarifa zake katika kituo kimoja tu.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva alisema tume hiyo imeshazifanyia majaribio mashine hizo katika majimbo matatu na zimeonyesha ubora na upungufu ulikuwa mdogo huku zile zenye kasoro zikifanyiwa marekebisho.
Chanzo MWANANCHI
COMMENTS