Falcao atoroka uwanjani
Mshambuliaji wa kimataifa wa Colombia na Manchester United, Radamel Falcao
HomeMichezo

Falcao atoroka uwanjani

Mshambuliaji wa kimataifa wa Colombia na Manchester United, Radamel Falcao MAJI ya shingo na hali si shwari. Ndivyo inavyoonekana kwa ...

MAJI ya shingo na hali si shwari. Ndivyo inavyoonekana kwa mshambuliaji wa kimataifa wa Colombia wa Manchester United, Radamel Falcao baada ya kupigwa benchi juzi na kuamua kuondoka uwanjani kwenda kutazama mechi nyumbani.

Staa huyo aliye kwa mkopo kutoka Monaco, aliachwa katika kikosi cha wachezaji18 kilichoiwakilisha United dhidi ya Southampton na kuchapwa bao 1-0 nyumbani Old Trafford.

Falcao anayelipwa Pauni 260,000 kwa wiki hakubaki uwanjani hapo na badala yake aliamua kuwasha gari lake na kuondoka zake uwanjani akitokomea kusikojulikana huku ikidhaniwa kuwa alikuwa amekwenda kutazamia mechi hiyo nyumbani baada ya kubaini kuwa hayupo katika mipango ya kocha.

Kutojumuishwa kikosini kwa Falcao kuliwashangaza wengi baada ya Kocha wa Man United, Van Gaal kukiri kwamba mshambuliaji huyo hakuwa majeruhi. Badala yake Van Gaal aliwaweka katika benchi walinzi watatu, Jonny Evans, Paddy McNair na Tyler Blackett huku katika safu ya ushambuliaji akimuweka benchi kinda James Wilson.

Falcao, ambaye ameanza mechi saba tu za Man United tangu alipojiunga kutoka Monaco, ameifungia Man United mabao mawili tu muhimu katika mechi zake tano zilizopita.
Katika mechi hizo aliipatia Man United pointi katika mechi dhidi ya Stoke City na AstonVilla, lakini sasa analazimika kupigania nafasi yake na pia kuhakikishaUnited inatoa dau la Pauni 45 milioni mwishoni mwa msimu kumchukua jumla.

Hata hivyo, Kocha Van Gaal amefafanua kwa nini alimuacha nje Falcao akidai kwamba zilikuwa sababu za kisoka zaidi na si vinginevyo.
“Inabidi uangalie mahitaji ya uchaguzi wako kwa wakati huo. Kama kocha inabidi uchukue maamuzi na inabidi uangalie mchanganyiko katika timu na pia inabidi uangalie mpango wako wa mechi,” alisema Van Gaal.

“Kwa hiyo niliamua kumuacha nje ya wachezaji 18 kwa sababu inabidi nifanye mabadiliko mfano ni Shaw na Di Maria,” aliongeza kocha huyo Mdachi.

Katika kikosi hicho United ilianza kwa kuwatumia mastaa wake wengine wote wanne katika safu ya ushambuliaji, Robin Van Persie, nahodha Wayne Rooney, Angel Di Maria na Juan Mata. Hata hivyo United ilitota kwa bao la Dusan Tadic katika dakika ya 69 ya mchezo huo.
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Falcao atoroka uwanjani
Falcao atoroka uwanjani
http://www.mwanaspoti.co.tz/image/view/-/2587524/highRes/920264/-/maxw/600/-/10fwhwgz/-/falcao_clip.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/falcao-atoroka-uwanjani.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/falcao-atoroka-uwanjani.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy