UNESCO Yaitambua Tanzania Kuwa Na Hifadhi Ya Nyaraka Za Kijerumani Ambazo Hazipatikani Sehemu Nyingine Yoyote Duniani
HomeHabari

UNESCO Yaitambua Tanzania Kuwa Na Hifadhi Ya Nyaraka Za Kijerumani Ambazo Hazipatikani Sehemu Nyingine Yoyote Duniani

  Na. James K. Mwanamyoto-Dar es Salaam Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Jenista Mhag...

Wadau wa Maonesho ya Mitindo Wahimizwa Kushiriki Katika Mageuzi ya Tasnia
Habari kubwa Magazetini Kenya leo March 2, 2025
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo March 2, 2025

 


Na. James K. Mwanamyoto-Dar es Salaam
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Jenista Mhagama amesema Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi, na Utamaduni (UNESCO) linatambua kuwa Tanzania kupitia Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa ina hifadhi kubwa ya nyaraka za utawala wa kijerumani ambazo hazipatikani sehemu nyingine yoyote duniani.

Waziri Jenista amesema hayo jijini Dar es Salaam alipokitembelea Kituo cha Kumbukumbu Kanda ya Mashariki na kujionea nyaraka hizo za kijerumani pamoja na taarifa hiyo ya UNESCO inayoitambua Tanzania kuwa na kumbukumbu za nyaraka muhimu za utawala wa Kijerumani.

Mhe. Jenista amesema, kitendo cha UNESCO kugundua kuwa Tanzania ina nyaraka muhimu za utawala wa kijerumani zisizopatikana sehemu nyingine duniani, ni jambo la kujivunia kama nchi kwani Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa imefanikiwa kuhifadhi nyaraka hizo ambazo zinalipa taifa heshima kubwa duniani ya utunzaji mzuri wa kumbukumbu za kihistoria.

“Sasa ni wakati muafaka na fursa adhimu ya kuzitangaza nyaraka hizi muhimu za kijerumani tulizozihifadhi ambazo zimepewa heshima ya kutambuliwa na UNESCO kama nyaraka muhimu na maalum ambazo hazipatikani mahali pengine duniani, ili ziweze kuwa kivutio kikubwa cha watalii nchini”, Mhe. Jenista amesisitiza.

Waziri Jenista ameongeza kuwa, Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa ya kutangaza vivutio vya watalii kupitia Royal Tour, hivyo Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa imuunge mkono kwa kutangaza amali hii ya nyaraka muhimu za utawala wa kijerumani ili kuongeza idadi ya watalii watakaoliongezea taifa kipato cha fedha za kigeni.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa, Bw. Firimin Msiangi, amesema nyaraka hizo za utawala wa iliyokuwa German East Africa (Tanganyika, Zanzibar, Burundi na Rwanda) ambayo Makao Makuu yake yalikuwa Dar es Salaam-Tanganyika ziliingizwa kwenye rejesta ya UNESCO ya mwaka 1997 ya Kumbukumbu ya Dunia na kutambuliwa rasmi kama sehemu ya Kumbukumbu ya Dunia (Memory of the World).

Aidha, Bw. Msiangi ameongeza kuwa idara yake ni ya huduma za nyaraka ambazo hazitumiki kwenye matumizi ya kawaida ya kila siku lakini zimethibitika kuwa na thamani endelevu katika historia ya taifa kwenye masuala ya kiutawala, kisheria, kiuchumi na kitafiti.

Akizungumzia mchakato wa upatikanaji wa nyaraka nyingine zinazohifadhiwa, Bw. Msiangi amesema sheria inaitaka Idara yake kufanya uchambuzi wa nyaraka kwenye Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Mamlaka na Taasisi nyingine za Umma ili kuzihifadhi katika eneo salama kwa sababu idara yake ina wataalam na vifaa vya vya kuifadhia.

Idara ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa inatekeleza shughuli zake kwa mujibu wa Sheria ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa Na. 3 ya mwaka 2002 na mnamo mwaka 2004 Bunge lilitunga Sheria Sheria Na. 18 ya Mwaka 2004 iliyoiongezea idara hiyo jukumu la Kuhifadhi Nyaraka za Waasisi wa Taifa (Mlm. J.K Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume).



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: UNESCO Yaitambua Tanzania Kuwa Na Hifadhi Ya Nyaraka Za Kijerumani Ambazo Hazipatikani Sehemu Nyingine Yoyote Duniani
UNESCO Yaitambua Tanzania Kuwa Na Hifadhi Ya Nyaraka Za Kijerumani Ambazo Hazipatikani Sehemu Nyingine Yoyote Duniani
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEguz9iXNP5as6c09IU6oDIInj0dNrgL8coAg0X7pmd0n0Cmid9Q_ZgVRWG-galvftN8EOXzu-bxvLNjIn2wS9GiNWK3QKYzytUv96jdFiOoWjx_4Xse43_FcXUd8ys4AHmZMJZSKR8s7_BfjhUPfwupMtlLr1KncWcjCw1BPh9jkMobOwjtWz1JH7VlSw/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEguz9iXNP5as6c09IU6oDIInj0dNrgL8coAg0X7pmd0n0Cmid9Q_ZgVRWG-galvftN8EOXzu-bxvLNjIn2wS9GiNWK3QKYzytUv96jdFiOoWjx_4Xse43_FcXUd8ys4AHmZMJZSKR8s7_BfjhUPfwupMtlLr1KncWcjCw1BPh9jkMobOwjtWz1JH7VlSw/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/05/unesco-yaitambua-tanzania-kuwa-na.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/05/unesco-yaitambua-tanzania-kuwa-na.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy