Waziri Mkuu Akagua Maandalizi Ya Siku Ya Mashujaa Dodoma

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan atakuwa Mgeni Rasmi katika maadhimisho ya siku ya Mashujaa, yat...

 


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan atakuwa Mgeni Rasmi katika maadhimisho ya siku ya Mashujaa, yatakayofanyika kitaifa Julai 25, 2022 Mkoani Dodoma.

Amesema hayo leo (Jumamosi, Julai 23, 2022), baada ya kukagua maandalizi ya maadhimisho hayo, katika viwanja vya Mashujaa Mkoani Dodoma. Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na maandilizi yaliyofanywa na kamati ya maadhimisho kitaifa kwa kushirikiana na vyombo vya Ulinzi na Usalama.

“Sherehe hii itafanyika kitaifa mkoani Dodoma na itaongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Viongozi wastaafu na viongozi wengine wa kitaifa.”

Waziri Mkuu amesema, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan aliridhia maadhimisho hayo yafanyike kitaifa mkoani Dodoma, lakini akaelekeza yafanyike nchi nzima kwa Wakuu wa Mikoa kuadhimisha siku hiyo kwa kwenda kwenye maeneo muhimu ya kumbukumbu kwenye mikoa yao.

“Kamati ya maadhimisho imefanya kazi yake vizuri sana kwa kushirikiana na vyombo vyote vya Ulinzi na Usalama, eneo linafafana na tukio lenyewe, lakini maandalizi ya vikundi mbalimbali ikiwepo vyombo vya ulinzi na usalama vimeleta askari kwa ajili ya gwaride, na mwaka huu  Jeshi la Uhamiaji limeanza kushiriki kikamilifu kwenye gwaride kuanzia kwenye tukio hili muhimu la mashujaa”

Aidha, Waziri Mkuu amevipongeza vyombo vya habari kwa namna ambavyo vimekuwa vikishiriki katika kutoa hamasa kwa wananchi kushiriki katika matukio mbalimbali ya kitaifa na kwamba Serikali inathamini mchango huo.

“Serikali inawashukuru sana wananchi kwa namna ambavyo wanajitokeza katika matukio haya ya kitaifa na kujanza viwanja, tunaamini pia Julai 25 watajitokeza kwa wingi.”


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends

COMMENTS

BLOGGER
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,2861,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri Mkuu Akagua Maandalizi Ya Siku Ya Mashujaa Dodoma
Waziri Mkuu Akagua Maandalizi Ya Siku Ya Mashujaa Dodoma
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEif2ywUqdGjkaCLzPOYIE1cQ2G-Hh2Z1yqQSOOI3HL5-jeh8_CudVlXGBX2arr9yGboEgDZVX0aBOGT751Sox19fLY1NR5RwAr-L_h0Q6XwP2QRkYxZDbEtAY3Xd8551qGmns45U9RaaOoIQ78wwVDsR8VvEICM8swAAZ6-giAfojpZQsoEOzgozKp_ig/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEif2ywUqdGjkaCLzPOYIE1cQ2G-Hh2Z1yqQSOOI3HL5-jeh8_CudVlXGBX2arr9yGboEgDZVX0aBOGT751Sox19fLY1NR5RwAr-L_h0Q6XwP2QRkYxZDbEtAY3Xd8551qGmns45U9RaaOoIQ78wwVDsR8VvEICM8swAAZ6-giAfojpZQsoEOzgozKp_ig/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
http://antagonf.blogspot.com/2022/07/waziri-mkuu-akagua-maandalizi-ya-siku.html
http://antagonf.blogspot.com/
http://antagonf.blogspot.com/
http://antagonf.blogspot.com/2022/07/waziri-mkuu-akagua-maandalizi-ya-siku.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy