Tanzania Na Kituo Cha Kudhibiti Magonjwa Nchini Marekani (CDC ) Kuendelea Kushirikiana

  Na. WAF Dar es Salaam Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania chini ya Rais Samia Sulu...

 


Na. WAF Dar es Salaam

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu Hassan itaendelea kushirikiana na Kituo cha Kudhibiti Magonjwa kutoka Marekani katika mapambano dhidi ya magonjwa mbalimbali.

Waziri Unmy amesema hayo mara baada kukutana na Mkurugenzi wa Kituo cha Udhibiti wa Magonjwa cha Marekani (CDC) Dkt. Rochelle Walensky na kufanya nae mazungumzo.

Waziri Ummy ameishukuru CDC kwa kuendelea kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia Mwaka 2001 katika kudhibiti magonjwa ya kuambukiza hususani ugonjwa wa UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria.

“Tumeshirikiana na CDC katika maneo mbalimbali yakiwemo; kuimarisha huduma za ufuatiliaji wa magonjwa, huduma Za maabara, kuwajengea uwezo wataalam kupitia mafunzo ya muda mfupi na mrefu na kuanzisha mfumo wa kidijitali katika kutoa mafunzo na kutafasiri majibu ya uchunguzi unaofanywa katika vituo vya ngazi ya msingi” amesema Waziri Ummy.

Aidha Mhe Ummy alimfahamisha Dkt Walensky kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan, ameweka kipaumbele katika masuala ya usalama wa afya hususani katika kujikinga, kufanya utambuzi na kukabiliana na mlipuko wa magonjwa na majanga.

Kuhusu UVIKO-19 Mhe Ummy ameipongeza CDC kwa kushirikiana na Serikali katika kukabiliana na mlipuko wa UVIKO-19 ikiwemo kuchangia katika kuongeza kasi ya uchanjaji wa chanjo ya UVIKO-19.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kituo cha kudhibiti magonjwa cha Marekani (CDC) Dkt. Rochelle Walensky Ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kuendelea kushirikiana kwa muda mwingi na kuahidi wataendelea kushirikiana kwa kujali Afya za watanzania pamoja na kuongeza msaada kwa Tanzania katika kudhibiti magonjwa na kulinda usalama wa watu duniani kote.

Dkt. Walensky amesema Kituo hicho hutumia ushahidi wa kisayansi katika kukabiliana na magonjwa hivyo ameishauri Serikali kupitia Wizara ya Afya kuongeza jitihada katika kufanya tafiti za kisayansi zinazohusiana na magonjwa na njia zinazotumika kukabiliana nayo.

Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends

COMMENTS

BLOGGER
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,2861,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Tanzania Na Kituo Cha Kudhibiti Magonjwa Nchini Marekani (CDC ) Kuendelea Kushirikiana
Tanzania Na Kituo Cha Kudhibiti Magonjwa Nchini Marekani (CDC ) Kuendelea Kushirikiana
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEixL89Qo4XesS2VQPHagkYdG0gyIVTRr5_jsH7vdXfLlle2l9XiZNhNbCfVo5dfh17C1H1uQerZufZATVLRAzGH0iMlbjass8zms9vxus_nXntKIowWl38rywDCvkh02Hif5tGWJwur8_g22ivx2ZaH0sZQKSMSS928lbFCknfwMPDYRZdypj6E4lOxAg/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEixL89Qo4XesS2VQPHagkYdG0gyIVTRr5_jsH7vdXfLlle2l9XiZNhNbCfVo5dfh17C1H1uQerZufZATVLRAzGH0iMlbjass8zms9vxus_nXntKIowWl38rywDCvkh02Hif5tGWJwur8_g22ivx2ZaH0sZQKSMSS928lbFCknfwMPDYRZdypj6E4lOxAg/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
http://antagonf.blogspot.com/2022/07/tanzania-na-kituo-cha-kudhibiti.html
http://antagonf.blogspot.com/
http://antagonf.blogspot.com/
http://antagonf.blogspot.com/2022/07/tanzania-na-kituo-cha-kudhibiti.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy