Serikali Yatoa Maelekezo Hatua Ya Kudhibiti Ajali Barabarani

 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Baraza la Taifa la Usalama Barabarani imetoa maelekezo yatayosaidia kudhibiti ajali ...


 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Baraza la Taifa la Usalama Barabarani imetoa maelekezo yatayosaidia kudhibiti ajali za barabarani nchini. Serikali imesema kuwa hairidhishwi na takwimu za ajali barabarani zilizotokea hivi karibuni na kutoa maelekezo matano kwa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, LATRA pamoja na watumiaji vyombo vya moto na abiria kwa ujumla.

Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Jumanne Sagini amesema kuwa Serikali ambayo inadhamana ya kulinda usalama wa raia na mali zao isingependa kuona matukio ya vifo na uharibifu wa mali za raia yakiendelea.

Naibu Waziri Sagini alielekeza LATRA na Kikosi cha Usalama Barabarani kupitia idadi ya magari madogo yaliyopewa leseni, kuendelea kufanya operesheni za kukamata magari yanayokiuka Sheria za Barabarani, kutoa elimu kwa abiria na wafanyabiashara wenye uwezo kuomba leseni za usafirishaji wa abiria kutoka LATRA kwenye maeneo ya uhitaji yakiwemo Mikoa ya Simiyu, Kagera, Kigoma, Mara na Geita.

“Serikali ambayo ina dhamana ya kulinda Usalama wa Raia na mali zao isingependa kuona matukio ya vifo na uharibifu wa mali za raia wake yakiendelea. Ni kwa msingi huo, tumemsikia mara kadhaa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akikemea na kulitaka Jeshi la Polisi kuchukua hatua madhubuti kudhibiti ajali za barabarani.

Naibu Waziri Sagini ameyasema hayo leo kwenye mkutano na waandishi wa Habari kuzungumzia masuala ya usalama barabarani uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Aidha ameipongeza Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Simiyu chini ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. David Kafulila kwa kuchukua hatua za kudhibiti matumizi ya magari yaliyosajiliwa kama teksi yanayokukiuka Sheria na kubeba abiria wengi na kwa masafa marefu.

“ Kamati hiyo ilichukua hatua hizo baada ya kujiridhisha kuwa magari hayo yamekuwa yakikiuka kwa kiwango kikubwa Sheria ya Usalama barabarani ikiwemo kubeba abiria wengi kuliko uwezo wa gari hizo, kuendesha magari kwa mwendo kasi kuliko inavyoruhusiwa” alisema.

Hatahivyo aliagiza Jeshi la Polisi, Kikosi cha Usalama Barabarani kuchukua hatua kwa askari Polisi mkoani Simiyu na nchini kwa ujumla watakaobainika wanamiliki tesksi hizo.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends

COMMENTS

BLOGGER
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,2861,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Serikali Yatoa Maelekezo Hatua Ya Kudhibiti Ajali Barabarani
Serikali Yatoa Maelekezo Hatua Ya Kudhibiti Ajali Barabarani
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh4xjPQ5f-ypEIU78tFXeB-v_siJrW494wNVAjZRxfAIH32A-zDtnYLr1utYWPEXQC0jaceNLgGlJEKCSanZKP4YDSMYYuGdVCsLIscS1rN8QP-X4XAdRMSAfGREzcJ1UMovmySwqUtFO2PIl_aZs0HJ4jU8nxSO4RaPk9gFrz2sXWGiFCd1X9JVdf8EA/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh4xjPQ5f-ypEIU78tFXeB-v_siJrW494wNVAjZRxfAIH32A-zDtnYLr1utYWPEXQC0jaceNLgGlJEKCSanZKP4YDSMYYuGdVCsLIscS1rN8QP-X4XAdRMSAfGREzcJ1UMovmySwqUtFO2PIl_aZs0HJ4jU8nxSO4RaPk9gFrz2sXWGiFCd1X9JVdf8EA/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
http://antagonf.blogspot.com/2022/07/serikali-yatoa-maelekezo-hatua-ya.html
http://antagonf.blogspot.com/
http://antagonf.blogspot.com/
http://antagonf.blogspot.com/2022/07/serikali-yatoa-maelekezo-hatua-ya.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy