Bashungwa aongoza Harambee Jimbo Katoliki Bunda,Mil 270 zakusanywa
HomeHabariTop Stories

Bashungwa aongoza Harambee Jimbo Katoliki Bunda,Mil 270 zakusanywa

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameshiriki Misa Takatifu katika Parokia ya Mtakatifu Paulo na kuongoza harambee ya kumalizia ujenzi wa ...

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameshiriki Misa Takatifu katika Parokia ya Mtakatifu Paulo na kuongoza harambee ya kumalizia ujenzi wa jengo la ofisi za Jimbo Katoliki la Bunda ambapo jumla ya Shilingi Milioni 272.6 imekusanywa.

Harambee hiyo imefanyika leo Novemba 10, 2024 Wilayani Bunda Mkoani Mara ambapo pamoja na mambo mengine, Waziri Bashungwa amezindua ofisi ya Askofu wa Jimbo Katoliki la Bunda, Mhashamu Simon Chibuga Msondole ambayo itaanza kutoa huduma za kijamii na kiroho.

“Jimbo letu la Bunda ni changa lina miaka 13, tunahitaji kubadilisha sura ya Jimbo letu, ili itakapofika Jubilei ya miaka 25, Jimbo liwe limepiga hatua kubwa na lenye kupendeza, lenye miundombinu mbalimbali kwa ajili ya huduma kwa watu wa Mungu na nchi yetu”, amesema Bashungwa

Bashungwa amelishukuru Kanisa Katoliki nchini kwa kuendelea kushirikiana na Serikali katika shughuli za ustawi na maendeleo ya jamii katika Sekta ya Elimu, Afya, na Sekta za uzalishaji hususani kilimo, uwekezaji katika viwanda, Hoteli pamoja na bima za aina mbalimbali.

Aidha, Bashungwa amemshukuru na kumpongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha miundombinu ya barabara, madaraja, mizani, vivuko na Kiwanja cha Ndege katika Mkoa wa Mara ambapo amebainisha baadhi ya miradi iliyokamilika, inayoendelea kutekelezwa na ambayo ipo katika hatua za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.

 

Akitaja miradi hiyo, Amesema ujenzi wa barabara ya Nyamuswa – Bulamba (km 56.4) umekamilika kwa kiwango cha lami kwa gharama ya Shilingi Bilioni 67.8 na kukamilika kwa ujenzi mzani wa kupima magari yakiwa kwenye mwendo (Weigh in Motion) katika eneo la Rubana kwa Shilingi Bilioni 22.2

Bashungwa amebainisha miradi mingine ni ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Sanzate – Nata (km 40) kwa gharama ya Shilingi Bilioni 51.08 ambao umefikia asilimia 55, ujenzi wa barabara ya Mogabiri – Nyamongo (km 25) kwa gharama ya shilingi Bilioni 34.6 na ujenzi umefikia asilimia 52.

Kadhalika, Bashungwa ameongeza kuwa Serikali inaendelea na ukarabati na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege Musoma kwa Shilingi Bilioni 35.048 na utekelezaji wake umefikia asilimia 57.

Kwa upande wake, Askofu wa Jimbo Katoliki la Bunda, Mhashamu Simon Chibuga Msondole amewashukuru viongozi wote wa Serikali, vyama vya kitume, waumini wa Parokia hiyo, marafiki na jamaa kwa majitoleo yao katika kufanikisha ujenzi wa ofisi za Parokia ya Bunda.

Naye, Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Chacha Maboto ametoa rai kwa uongozi wa Jimbo Katoliki la Bunda kuhakikisha wanasimamia kikamilifu michango yote iliyotolewa katika harambee hiyo ili ziweze kutimiza malengo yaliyokusudiwa.

Akisoma Risala, Mwenyekiti wa Kamati ya Harambee Jimbo la Bunda, Kulwa Kahabi amesema kuwa harambee hiyo imehusisha waumini wa Parokia 23, vyama vya kitume, watu binafsi na kufafanua harambee hiyo imekusanywa kwa awamu ambapo awamu ya kwanza mwaka 2022 na walikusanya Milioni 240, awamu ya pili mwaka 2023 walikusanya Milioni 130 na katika mwaka 2024 matarajio yao ni kukusanya Milioni 350.

 

 

The post Bashungwa aongoza Harambee Jimbo Katoliki Bunda,Mil 270 zakusanywa first appeared on Millard Ayo.



from Millard Ayo https://ift.tt/30Kw4BS
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Bashungwa aongoza Harambee Jimbo Katoliki Bunda,Mil 270 zakusanywa
Bashungwa aongoza Harambee Jimbo Katoliki Bunda,Mil 270 zakusanywa
https://millardayo.com/wp-content/uploads/2024/11/IMG-20241111-WA0019-950x633.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2024/11/bashungwa-aongoza-harambee-jimbo.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2024/11/bashungwa-aongoza-harambee-jimbo.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy