RC Serukamba -Elimu ndio nguzo ya maendeleo ya jamii na uchumi
HomeHabariTop Stories

RC Serukamba -Elimu ndio nguzo ya maendeleo ya jamii na uchumi

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba amehimiza Wazazi na Walezi Nchini kuhakikisha watoto wao wanapata Elimu na kuwahimiza watoto hao...

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba amehimiza Wazazi na Walezi Nchini kuhakikisha watoto wao wanapata Elimu na kuwahimiza watoto hao juu ya Umuhimu wa Elimu kwani Elimu ndio Nguzo ya maendeleo ya jamii na Uchumi

Ameyasema hayo leo wakati akihutubia kwenye mahafali ya wanafunzi wa Shule ya Real Hope iliyopo katika Halmashauri ya Mji Mafinga Wilaya ya Mufindi.

Mhe Serukamba Amesema kuwa jambo kubwa ambalo watoto wanatakiwa kurithi kutoka kwa wazazo wao ni Elimu hivyo wazazi wametakiwa kulipa kipaumbele suala la elimu ili kuleta maendeleo katika jamii

Aidha Mhe. Serukamba ameongeza kwa kuwataka wasomi wote kujijengea tabia ya kujifunza kila siku kwa kusoma vitabu mbalimbali kwani kwa sasa sayansi na teknolojia ikekuwa kwa kasi tofauti na hapo awali.

Vile vile Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mh. Peter Serukamba, ameutaka uongozi wa Shule ya Real Hope pamoja na Kamati ya Shule hiyo kujenga maktaba kubwa ya vitabu kwa ajili ya wanafunzi kujisomea. Amesema kuwa, hivi sasa, wanafunzi wengi wamekuwa wavivu wa kusoma vitabu, hali inayopelekea uwezo mdogo wa fikra.

Mh. Serukamba alisisitiza kuwa licha ya juhudi kubwa wanazofanya walimu katika kufundisha na kuwasaidia wanafunzi kufaulu, bado kuna haja ya kujenga maktaba ili kuwapa fursa wanafunzi kujisomea zaidi.

Mkurugenzi wa shule hizo, Bw. Dickson Mwipopo, aliongeza kuwa ni muhimu kwa wazazi kuendeleza mafunzo na maadili mema kwa watoto wao, akisisitiza kwamba mapinduzi dhidi ya ukatili wa kijinsia na matukio mabaya ya uhalifu yatakoma pale wazazi watakapowaelekeza watoto katika misingi ya maadili mazuri waliyopata shuleni.

The post RC Serukamba -Elimu ndio nguzo ya maendeleo ya jamii na uchumi first appeared on Millard Ayo.



from Millard Ayo https://ift.tt/8EhGnIH
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: RC Serukamba -Elimu ndio nguzo ya maendeleo ya jamii na uchumi
RC Serukamba -Elimu ndio nguzo ya maendeleo ya jamii na uchumi
https://millardayo.com/wp-content/uploads/2024/09/IMG-20240921-WA00111-950x633.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2024/09/rc-serukamba-elimu-ndio-nguzo-ya.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2024/09/rc-serukamba-elimu-ndio-nguzo-ya.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy