Mtendaji Mkuu Mahakama Atoa Wito Kwa Wananchi Kuandika Wosia
HomeHabari

Mtendaji Mkuu Mahakama Atoa Wito Kwa Wananchi Kuandika Wosia

  Na Mary Gwera, Mahakama Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole Gabriel ametoa wito kwa wananchi hususani wanaume ku...

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo February 2
Wabunge Wampitisha Tulia Ackson Kiti Cha Uspika Kwa Kura 376
Rais Samia Suluhu amemteua Zuhura Yunus kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais - Ikulu.

 


Na Mary Gwera, Mahakama

Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole Gabriel ametoa wito kwa wananchi hususani wanaume kuandika wosia ili kuepusha migogoro mbalimbali ikiwemo ya kugombea mali kwa familia wanazoziacha.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijni Dar es Salaam  tarehe 08 Julai, 2022 alipotembelea banda la Mahakama ya Tanzania lililopo katika Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ‘Sabasaba’, Prof. Ole Gabriel amesema kuwa familia nyingi hususani wajane na watoto wamekuwa wakikabiliana na migogoro ya kugombea mali zilizoachwa na marehemu.

“Wajane wengi wanakabiliwa na migogoro kutoka kwa ndugu pindi mume anapofariki, hivyo ni rai yangu kwa Watanzania na haswa wanaume wenzangu kuandika wosia ili kuepusha matatizo yanayotokea kwa mjane na Watoto,” amesema Prof. Ole Gabriel.

Mtendaji Mkuu ameongeza kuwa katika jitihada za kuhakikisha kuwa Mahakama inashughulikia kwa ukaribu masuala ya familia ikiwemo Mirathi, Mahakama ilianzisha kituo maalum cha kushughulikia masuala ya familia hivyo kuwataka wananchi kutosita kupata huduma zinazotolewa katika kituo hicho.

Aidha; Mtendaji Mkuu amesema katika kipindi cha Maonesho ya ‘sabasaba’ moja ya huduma zinazotolewa katika banda la Mahakama ni pamoja na kutoa elimu ya Wosia na Mirathi hivyo ni vyema wananchi watembelee banda hilo ili kujua zaidi.

Kwa upande mwingine, Mtendaji Mkuu huyo amewakumbusha wananchi kuendelea kutumia namba ya huduma kwa mteja ya Mahakama ‘Call Centre’ ambayo ni 0752 500 400 ili kupata utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazowasibu kuhusu Mahakama.

“Tumeanzisha hii ‘call centre’ maalum kwa ajili ya kuwahudumia wananchi, unapokutana changamoto yoyote usimpigie Jaji Mkuu au Jaji Kiongozi au Msajili Mkuu bali piga namba 0752 500 400 inayopatikana masaa 24,” amesema Mtendaji Mkuu.

Mahakama ya Tanzania ni moja ya Taasisi zinazoshiriki katika Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa lengo ni kutoa elimu kwa wananchi kuhusu taratibu na huduma inazotoa.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Mtendaji Mkuu Mahakama Atoa Wito Kwa Wananchi Kuandika Wosia
Mtendaji Mkuu Mahakama Atoa Wito Kwa Wananchi Kuandika Wosia
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiNgJpeIhKLOFUZwCnVYZAS_xZHNAaPLdXjuuu65c-9DLf6vskwbJVgHTp66yn48ZXbSfAXI8t5rRsRqS-oDmdxY7X75qt00ch9baRR5e8f_r-FuFfyvx6yX9zC1i-0YUEtSQl1ooPYx3h1Y3sgKEbxFXp6GnL8nN1HoTFks7dGV8WE3jLD34Bsze1HXw/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiNgJpeIhKLOFUZwCnVYZAS_xZHNAaPLdXjuuu65c-9DLf6vskwbJVgHTp66yn48ZXbSfAXI8t5rRsRqS-oDmdxY7X75qt00ch9baRR5e8f_r-FuFfyvx6yX9zC1i-0YUEtSQl1ooPYx3h1Y3sgKEbxFXp6GnL8nN1HoTFks7dGV8WE3jLD34Bsze1HXw/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/07/mtendaji-mkuu-mahakama-atoa-wito-kwa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/07/mtendaji-mkuu-mahakama-atoa-wito-kwa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy