Jeshi la Sudan lashambulia eneo linalozozaniwa katika mpaka na Ethiopia
HomeHabari

Jeshi la Sudan lashambulia eneo linalozozaniwa katika mpaka na Ethiopia

Majeshi ya Sudan yalifyatua mizinga mikubwa wakati wa mapigano katika eneo la mashariki linalozozaniwa la al-Fashaqa linalopakana n...

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo February 26
Rais Magufuli avunja Jiji la Dar es Salaam
Wakandarasi Watakao Chelewesha Miradi Ya Maji Kutoongezewa Muda


Majeshi ya Sudan yalifyatua mizinga mikubwa wakati wa mapigano katika eneo la mashariki linalozozaniwa la al-Fashaqa linalopakana na Ethiopia.

Hayo yamedokezwa na afisa wa Ethiopia huku kukiwa na wasiwasi wa kuibuka tena mvutano baina ya nchi hizo mbili kuhusu  mzozo wa muda mrefu katika eneo hilo la mpaka wa pamoja.

Jumanne Sudan iliweza kuteka eneo la Jabal Kala al-Laban, lililo karibu na mpaka unaozozaniwa, kufuatia shambulio la anga, kwa mujibu wa afisa wa  kijeshi wa Sudan ambaye hakutajwa jina akizungumza na shirika la habari la Reuters.

Siku ya Jumatatu, Ethiopia ilikanusha shutuma za Sudan kwamba jeshi lake lilikamata na kuwanyonga wanajeshi saba wa Sudan na raia mmoja, badala yake ikasema mauaji hayo yametekelezwa na wanamgambo wa eneo hilo.

Duru za serikali ya Sudan zilisema kuwa Sudan imewasilisha malalamiko rasmi kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu mauaji hayo.

Jeshi la Sudan lilifyatua mizinga ya masafa marefu kuanzia Jumatatu asubuhi hadi Jumanne alasiri, lakini hakuna aliyejeruhiwa, alisema Assefa Ashege, afisa mkuu wa usalama katika eneo la Amhara nchini Ethiopia.

Wakaazi wawili wa eneo hilo walisema kuwa jeshi la Sudan limechukua udhibiti wa eneo la Jabal Kala al-Laban.

Mzozo kuhusu al-Fashaqa, ambayo ipo ndani ya mipaka ya kimataifa ya Sudan lakini imekaliwa na wakulima wa Ethiopia kwa miongo kadhaa, umeongezeka katika miaka ya hivi karibuni sambamba na mzozo wa kidiplomasia kuhusu ujenzi wa Ethiopia wa bwawa la kufua umeme wa maji.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Jeshi la Sudan lashambulia eneo linalozozaniwa katika mpaka na Ethiopia
Jeshi la Sudan lashambulia eneo linalozozaniwa katika mpaka na Ethiopia
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEie34JQiy_3DOK0UbNHmvgDK5WAwAo-D72aXj4JrQI0rcSF5xw2h-eyicSB_pYdeSmsw_DMkKQ_DaAnsjFYrU9kDujvuJXCcOmDX3uh8cOz6fHUf5xu5avrap1JpMXbTm3lDHYJ9UrnzC3Gno3Q1CXSnHIOkID5m1SBQlr-aPybWMlmv97TPc3mLDZCEQ/s16000/7333c975-1b14-474d-b4b1-7db2c0b0adba.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEie34JQiy_3DOK0UbNHmvgDK5WAwAo-D72aXj4JrQI0rcSF5xw2h-eyicSB_pYdeSmsw_DMkKQ_DaAnsjFYrU9kDujvuJXCcOmDX3uh8cOz6fHUf5xu5avrap1JpMXbTm3lDHYJ9UrnzC3Gno3Q1CXSnHIOkID5m1SBQlr-aPybWMlmv97TPc3mLDZCEQ/s72-c/7333c975-1b14-474d-b4b1-7db2c0b0adba.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/06/jeshi-la-sudan-lashambulia-eneo.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/06/jeshi-la-sudan-lashambulia-eneo.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy