Bajeti ya trilioni 14.94 Wizara ya fedha yapita
HomeHabari

Bajeti ya trilioni 14.94 Wizara ya fedha yapita

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha bajeti ya wizara ya Fedha kwa mwaka wa fedha wa 2022/2023 ya shilingi trilioni 14.94...


Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha bajeti ya wizara ya Fedha kwa mwaka wa fedha wa 2022/2023 ya shilingi trilioni 14.94.

Fedha hizo ni kwa ajili ya kugharamia matumuzi ya kawaida na maendeleo kwa mwaka huo wa fedha wa 2022/2023.

Akiwasilisha bajeti ya wizara ya Fedha kwa mwaka wa fedha wa 2022/2023 bungeni jijini Dodoma, Waziri wa wizara hiyo Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kati ya fedha hizo shilingi trilioni 13.6 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na trilioni 1.3 ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.

Kuhusu usimamizi na udhibiti wa ununuzi wa umma Dkt. Nchemba ameliambia Bunge kuwa watafanya mapitio na ujenzi wa mfumo mpya wa usimamizi wa ununuzi wa umma na kufuatilia utekelezaji wa mikataba ya ununuzi katika taasisi nunuzi.

“Katika mwaka wa fedha 2022/23, Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma – PPRA inatarajia kuanza ujenzi wa ofisi ya Makao Makuu jijini Dodoma na ofisi ya kanda jijini Dar es Salaam, kuwezesha mafunzo kwa watumishi 940 kutoka katika Taasisi Nunuzi 170 na wazabuni 1,200 ambao wamejisajili katika mfumo wa TANePS, kufanya mapitio na ujenzi wa mfumo mpya wa usimamizi wa ununuzi wa umma na kufuatilia utekelezaji wa mikataba ya ununuzi katika Taasisi Nunuzi 530” amesema Dkt. Nchemba

Amefafanua kuwa katika mwaka wa fedha wa 2022/2023, wizara ya Fedha inakadiria kukusanya maduhuli ya jumla ya shilingi trilioni 1.05 kutoka katika vyanzo mbalimbali ikiwa ni pamoja na gawio, kodi za pango, marejesho ya mikopo, michango kutoka katika taasisi na mashirika ya umma pamoja na mauzo ya leseni za udalali.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Bajeti ya trilioni 14.94 Wizara ya fedha yapita
Bajeti ya trilioni 14.94 Wizara ya fedha yapita
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgPAu0kCDZbRe7fJDRvzzXGkhB7eZ67qhOfMP_PrtOxswCGPddN78qgvwq3bdw9JA7nw8XLLh30tdSocfAd6T1TNOuy0n9A2kLxFOMCxia3puIwvibrv8k2GGrJuk7qQ6sV_uGqglNHmT5cjICofgRhqinikQqn5gwi106xBY2fCrel0qJVuBt4yJRDLA/s16000/103A3036-1-1024x683.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgPAu0kCDZbRe7fJDRvzzXGkhB7eZ67qhOfMP_PrtOxswCGPddN78qgvwq3bdw9JA7nw8XLLh30tdSocfAd6T1TNOuy0n9A2kLxFOMCxia3puIwvibrv8k2GGrJuk7qQ6sV_uGqglNHmT5cjICofgRhqinikQqn5gwi106xBY2fCrel0qJVuBt4yJRDLA/s72-c/103A3036-1-1024x683.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/06/bajeti-ya-trilioni-1494-wizara-ya-fedha.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/06/bajeti-ya-trilioni-1494-wizara-ya-fedha.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy