China yawaasa viongozi wa Marekani wachunge kauli zao kuhusiana na Taiwan
HomeHabari

China yawaasa viongozi wa Marekani wachunge kauli zao kuhusiana na Taiwan

China imetoa jibu kali dhidi ya uingiliaji wa waziwazi wa Marekani katika masuala ya ndani ya nchi hiyo. Beijing imewaasa viongozi wa...


China imetoa jibu kali dhidi ya uingiliaji wa waziwazi wa Marekani katika masuala ya ndani ya nchi hiyo. Beijing imewaasa viongozi wa Washington wachunge kauli wanazotoa kuhusiana na Taiwan.

Katika kile kinachoonekana kuwa ni uingiliaji wa masuala ya ndani ya China, Rais Joe Biden wa Marekani ambaye jana alikuwa ziarani nchini Japan alitangaza waziwazi uungaji mkono wake kwa Taiwan na kutamka kwamba: "ikiwa China itaishambulia Taiwan, Marekani itaisaidia na kuiunga mkono kijeshi Taiwan."

Akiwa mjini Tokyo, Biden aliongezea kwa kusema: "sisi tumetoa ahadi kuhusiana na Taiwan. Utumiaji wowote wa mabavu na ulazimishaji wa China dhidi ya Taiwan haufai na utachukuliwa kuwa ni kitu kisichokubalika. Kwa hatua zake, China inauathiri ukanda mzima na kitakachojiri hali sawa na iliyotokea Ukraine."

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China amejibu matamshi hayo ya rais wa Marekani kuhusiana na Taiwan kwa kusema: "kadhia ya Taiwan na Ukraine ziko tofauti kabisa; na si sahihi kuzilinganisha hata kidogo."

Zhao Lijian ameongezea kwa kusema: "Taiwan ni sehemu ya ardhi ya China na sisi hatuiruhusu nchi yoyote iingilie masuala yetu ya ndani."

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China amegusia pia kauli kali ya vitisho aliyotumia Joe Biden dhidi ya nchi yake na akasema:"Marekani inatambua kwamba China inao uwezo wa kulinda ardhi yake."

Serikali ya Beijing imekuwa ikisisitiza kuwa kadhia ya Taiwan haina chochote cha kulinganishwa na kinachoendelea Ukraine ikisistiza kuwa kisiwa cha Taiwan ni sehemu ya ardhi kuu ya China.

China imeshaionya Marekani mara kadhaa kwamba haitakuwa tayari kufanya maridhiano yoyote juu ya suala la Taiwan na itatoa jibu kali kwa chokochoko zozote zitakazofanywa juu ya suala hilo



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: China yawaasa viongozi wa Marekani wachunge kauli zao kuhusiana na Taiwan
China yawaasa viongozi wa Marekani wachunge kauli zao kuhusiana na Taiwan
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhcl1gWLMd6QUthB2IZJlb9MdT76dJrILZyikRYWquhFsmBpsGB5GBDSLSGiWAo_iCZnqHtPDI2OTmQdiX8w_o2AIdnn5IqJcDatgBmTxpBcaNJh0tE0yjx3Px68kG9cS19rLUlbfXQdovxsXsvbl6SkE1rSPmAKakS63NTzSuE7QZjEfjlb2_bPonoIw/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhcl1gWLMd6QUthB2IZJlb9MdT76dJrILZyikRYWquhFsmBpsGB5GBDSLSGiWAo_iCZnqHtPDI2OTmQdiX8w_o2AIdnn5IqJcDatgBmTxpBcaNJh0tE0yjx3Px68kG9cS19rLUlbfXQdovxsXsvbl6SkE1rSPmAKakS63NTzSuE7QZjEfjlb2_bPonoIw/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/05/china-yawaasa-viongozi-wa-marekani.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/05/china-yawaasa-viongozi-wa-marekani.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy