Magari 4,041 yashushwa bandari ya Dar es Salaam
HomeHabari

Magari 4,041 yashushwa bandari ya Dar es Salaam

Bandari ya Dar es Salaam imeandika historia mpya baada ya kupokea kwa mara moja magari 4,041. Akizungumza katika hafla ya mapokezi ya m...

Malkia wa Uingereza akutwa na corona baada ya kupimwa
Putin, Macron na Zelensky wajadili mgogoro wa eneo la mashariki ya Ukraine
Tanzania Bara, Zanzibar Kutekeleza Kwa Pamoja Anwani Za Makazi


Bandari ya Dar es Salaam imeandika historia mpya baada ya kupokea kwa mara moja magari 4,041.

Akizungumza katika hafla ya mapokezi ya meli iliyobeba magari hayo Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema tangu kukarabatiwa kwa gati namba 1 hadi 7 iliyogharimu Trioni moja imesaidia kuongeza idadi ya magari yaliyokuwa yakishushwa kutoka magari 700 hadi 4000 na zaidi kwa siku.

Profesa Mbarawa amesisitiza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuwa magari yote yanayoagizwa kukaguliwa huko yanakotoka yakifika Tanzania yatoke bila kukaguliwa ili kuepuka msongamano wa magari bandarini.

“Nataka nisisitize agizo la Rais wetu kuwa magari yote yakaguliwe huko huko yanakotoka kuepuka msongamano wa magari bandarini na niwatake mamlaka ya bandari kuwa na timu ya masoko iende huko nchi zingine kuitangaza bandari yetu kwa huduma bora inazotoa hasa usalama wa bandari yetu” amesema Profesa Mbarawa

Aidha Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Eric Hamissi amesema gari hizo zilizoshushwa leo gari 1105 sawa na asilimia 27% ni za hapa nchini na gari 2936 sawa na asilimia 73% zinakwenda nchi jirani kama Sudan Kusini, Zimbabwe, Msumbiji na Malawi

Eric ameongeza kuanzia tarehe 5 hadi 7 Aprili (Siku tatu) wamepokea meli nne zenye jumla ya magari 8384 ukilinganisha na mwaka uliopita walikuwa wakipokea gari 10,000 kwa mwezi mmoja

“Meli hii imetumia muda wa siku 19 ikitoka Japan hadi Tanzania ukilinganisha na kipindi cha nyuma meli ilikuwa ikitumia siku 40 na niseme meli zingine mbili zitaingia mwezi huu Aprili zikiwa na jumla ya magari 2000”




Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Magari 4,041 yashushwa bandari ya Dar es Salaam
Magari 4,041 yashushwa bandari ya Dar es Salaam
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg_59PxLxVaSeUfJe57j0OvTa-toSa-yvOcsedotZiulrpd6se0gyM5RxZAhPKnWN80q5XUArWR33iBAR6rVLwWAOO2juZHNSxJAGZHATvm1vlYUsu1bb3cEfJ6kSQW6764kE55fOgBhiUrk56wCWxKH1dEfTsJjAkMAFloU3MEmKOA7GUxeKeAlh-2bw/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg_59PxLxVaSeUfJe57j0OvTa-toSa-yvOcsedotZiulrpd6se0gyM5RxZAhPKnWN80q5XUArWR33iBAR6rVLwWAOO2juZHNSxJAGZHATvm1vlYUsu1bb3cEfJ6kSQW6764kE55fOgBhiUrk56wCWxKH1dEfTsJjAkMAFloU3MEmKOA7GUxeKeAlh-2bw/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/04/magari-4041-yashushwa-bandari-ya-dar-es.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/04/magari-4041-yashushwa-bandari-ya-dar-es.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy