Washtakiwa saba wa kesi ya mauaji ya mfanyabiashara wa madini ambao ni maofisa wa polisi mkoani hapa, wamesema hawakuwahi kuingia mkataba...
Washtakiwa saba wa kesi ya mauaji ya mfanyabiashara wa madini ambao ni maofisa wa polisi mkoani hapa, wamesema hawakuwahi kuingia mkataba na wakili yeyote wa utetezi, ila muda mwafaka ukifika watafanya hivyo.
Washtakiwa hao walieleza hayo katika Mahakama ya Hakimu mkazi Mtwara juzi ambapo kesi hiyo ilifika kwa ajili ya kutajwa, mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Makahama hiyo, Lugano Kasebele.
Mshtakiwa wa kwanza katika kesi hiyo, aliyekuwa Mkuu wa upelelezi Wilaya ya Mtwara, Gilbert Kalanje aliieleza Mahakama hiyo kuwa yeye binafsi hajawahi kuingia mkataba na wakili yeyote.
“Mheshimiwa hakimu katika kumbukumbu zako naomba ieleweke kwamba mimi kama mshtakiwa namba moja, sijawahi kuingia mkataba wala kuongea na wakili yeyote, ikifika muda mwafaka nitafanya hivyo, vilevile tunaomba tupatiwe hati ya mashtaka,” alisema Kalanje.
Mara baada ya kusema hivyo, washtakiwa wengine wote nao waliieleza Mahakama hiyo kuwa hawajawahi kuingia mkataba na wakili yeyote.
Kalanje alitoa ufafanuzi huo mara baada ya hakimu Kasebele kuaihirisha kesi hiyo hadi Machi 22, 2022 itakapotajwa tena.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuahirisha kesi hiyo, Hakimu Kasebele alisema kauli ya washtakiwa hao imeisaidia Mahakama kujua kuwa hawakuwahi kuwa na wakili yeyote.
Credit: MPEKUZI
Thanks for your time please share with your friends
COMMENTS