Tanzania Yafafanua Msimamo Wake Kuhusu Mgogoro Wa Urusi Na Ukraine
HomeHabari

Tanzania Yafafanua Msimamo Wake Kuhusu Mgogoro Wa Urusi Na Ukraine

 Na Mwandishi Wetu, Dar Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa ufafanuzi kuhusu sababu ya kupiga kura ya kutofungamana na upande wowote ...


 Na Mwandishi Wetu, Dar
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa ufafanuzi kuhusu sababu ya kupiga kura ya kutofungamana na upande wowote katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu mgogoro unaoendelea kati ya Urusi na Ukraine huku ikisisitiza pande zote mbili kutafuta suluhu katika meza ya mazungumzo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) ametoa ufafanuzi huo wakati akifanya mahojiano na mojawapo ya vyombo vya Habari kutoka China na kuongeza kuwa Sera ya Tanzania kuhusu namna ya kutatua changamoto za migogoro inapojitokeza ni kwa kutumia njia za kidiplomasia.

Balozi Mulamula amesisitiza kuwa Sera ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haijabadilika tangu uhuru na kuongeza kuwa Tanzania inaamini hakuna mgogoro ambao hauwezi kutatulika  hasa panapokuwepo na utashi na nia njema ya kumaliza mgogoro na kwamba njia ya kidiplomasia ndio chaguo sahihi kwa Tanzania kuhusu namna bora ya kumaliza mgogoro  kati ya Urusi na Ukraine.

“Sisi msimamo wetu na Sera yetu na msingi wetu wa Sera yetu ya Mambo ya Nje ni kutofungamana na pande zozote, hivyo kutokupiga kura ni kuonesha msimamo wa Tanzania,” amesema Balozi Mulamula

Alipoulizwa endapo Tanzania imeathirika na vita inayoendelea kati ya Urusi na Ukraine, Balozi Mulamula amesema madhara yanayotokana na vita hiyo yanajionesha dhahiri huku akitaja baadhi ya madhara hayo kwa baadhi ya wanafunzi wa kitanzania waliokuwa wanasoma nchini Urusi kukatisha masomo yao na kurejea nchini wakisubiria vita kumalizika pamoja na ongezeko la bei ya petroli na gesi duniani.

Kutokana na vita inayoendelea kati ya Ukraine na Urusi Tanzania ililazimika kuwaondoa raia wake nchini Ukraine hususan wanafunzi takribani 300 waliokuwa wakisomea masuala ya udaktari nchini humo


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Tanzania Yafafanua Msimamo Wake Kuhusu Mgogoro Wa Urusi Na Ukraine
Tanzania Yafafanua Msimamo Wake Kuhusu Mgogoro Wa Urusi Na Ukraine
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi2w3ubkDAxoY3a6wESPgKylkVNHyWYn-vrWn_tskQJ0Dh7GdDLQSh5RZlg4d2ekK55t9VpDodG9uEykSgB_0kJ9dXsrV9I7sGe-Se9TpVSCDGo76Xr-iJZc5QWvo6ftB1i2vgGFPLL7-g1sWJ7us8R-F7fsLMQtxcuooV95Jo-j1_txeIPDoAZbVe_pg/s16000/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi2w3ubkDAxoY3a6wESPgKylkVNHyWYn-vrWn_tskQJ0Dh7GdDLQSh5RZlg4d2ekK55t9VpDodG9uEykSgB_0kJ9dXsrV9I7sGe-Se9TpVSCDGo76Xr-iJZc5QWvo6ftB1i2vgGFPLL7-g1sWJ7us8R-F7fsLMQtxcuooV95Jo-j1_txeIPDoAZbVe_pg/s72-c/1.JPG
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/03/tanzania-yafafanua-msimamo-wake-kuhusu.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/03/tanzania-yafafanua-msimamo-wake-kuhusu.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy