Ridhiwani Kikwete Ataka Mipaka Ya Ardhi Iheshimiwe Kuepuka Migogoro
HomeHabari

Ridhiwani Kikwete Ataka Mipaka Ya Ardhi Iheshimiwe Kuepuka Migogoro

Na   Magreth Lyimo na Hassan Mabuye WANMM PWANI   Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete ametaka kuhesh...

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne February 10
Serikali yaombwa kusitisha tozo za utalii
Hotuba Ya Mapendekezo Ya Mwongozo Wa Maandalizi Ya Mpango Na Bajeti Ya Serikali Na Mpango Wa Maendeleo Wa Taifa Kwa Mwaka 2021/22


Na Magreth Lyimo na Hassan Mabuye WANMM PWANI

 

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete ametaka kuheshimiwa kwa mipaka ya ardhi baina ya kijiji na kijiji ili kuepuka migogoro.

 

Alisema, mipaka ya vijiji imewekwa ili kuwezesha utoaji bora wa huduma kwenye jamii husika na wananchi hawapaswi kugombania rasilimali ardhi hiyo. 

 

Ridhiwani ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze mkoani Pwani alisema hayo tarehe 2/3/2022 alipoanza ziara ya  kusikiliza na kutolea ufafanuzi changamoto mbalimbali katika jimbo lake ikiwamo migogoro ya ardhi ambapo katika siku yake ya kwanza  ya ziara yake alitembelea kata ya Miono na kufanya mikutano kwenye Vijiji vitatu vya Kweikonje, Masimbani pamoja na Miono mjini. 

  

‘‘Kila mtanzania ana haki ya kumiliki ardhi sehemu yoyote nchini lakini kwa watu wanaotoka nje ya kijiji husika wanapaswa kufuata sheria na taratibu ikiwamo kuwasilisha maombi ofisi ya Mwenyekiti wa Kijiji na baada ya hapo mkutano mkuu wa kijiji uitwe ili kijiji kiridhie kumpa ardhi hiyo muombaji’’ alisema Ridhiwani Kikwete.

 

Kauli hiyo ya Ridhiwani inafuatia mwananchi mmoja kutoka mkoa mwingine anayeishi kijiji cha Masimbani Kata ya Miono mkoa wa Pwani  kuomba kibali cha kumiliki ardhi katika kijiji hicho na  kuishia kuzungushwa na uongozi wa kijiji. 

 

Katika kikao hicho, ilionekana pia kuna migogoro mingi kati ya wafugaji na wakulima sambamba na migogoro ya mipaka ambapo Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa wa Pwani Bi. Lucy Kabyemera alieleza kuwa  kila kijiji ni lazima kipimwe ili mpango wa matumizi bora ya ardhi uweze kuandaliwa alioueleza kuwa utasaidia kuepusha migogoro hiyo ya ardhi.

 

‘‘Kwa kukamilisha zoezi la upimaji haraka itasaidia kuandaa Mpango wa Matumizi bora ya ardhi na kila aliyepimiwa ana haki ya kuandaliwa hatimiliki ya kimila itakayomuhakikishia usalama wa milki yake. Katika zoezi hilo elimu pia itatolewa ili wananchi wajue umuhimu wa kupata hati kwenye  eneo wanayoishi’’ alisema Kabyemera.

 

Mmoja wa wananchi waliohudhuria mikutano hiyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Bw. Kawambwa alisema kuwa, wananchi wanahitaji kupimiwa maeneo yao ili waweze kupata hati ambazo zitawasaidia kupata mikopo aliyoieleza kuwa itasaidia kuongeza nguvu kwenye biashara zao.

 

Kupitia mkutano huo, wananchi wa Kata ya Maono walisisitizwa pia kutoa ushirikiano, kujitokeza kwa wingi pamoja na kutoa taarifa sahihi kwenye zoezi la Anwani za Makazi linalotegemea kuanza mapema mwezi huu wa tatu 2022 ambapo vijana kwenye mitaa watatumika kukusanya taarifa hizo.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Ridhiwani Kikwete Ataka Mipaka Ya Ardhi Iheshimiwe Kuepuka Migogoro
Ridhiwani Kikwete Ataka Mipaka Ya Ardhi Iheshimiwe Kuepuka Migogoro
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiedl2k1By_xHPGxxUkrYkLvGp7szD_pEGWqEQWIvvXXh-GVm5XV00OJkA9mXnNweKl2YG0eplSfjD3pvcRdhzPBQRiCIXKeLsgIBxjWj4T3Ob-XuVCNq1zk2BuPxkDsppxL7CnHtSr43dEOy2GNETRHD9pHto8X8LO-cY3rqHw3lV_yt4swJRnL4hw2g=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiedl2k1By_xHPGxxUkrYkLvGp7szD_pEGWqEQWIvvXXh-GVm5XV00OJkA9mXnNweKl2YG0eplSfjD3pvcRdhzPBQRiCIXKeLsgIBxjWj4T3Ob-XuVCNq1zk2BuPxkDsppxL7CnHtSr43dEOy2GNETRHD9pHto8X8LO-cY3rqHw3lV_yt4swJRnL4hw2g=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/03/ridhiwani-kikwete-ataka-mipaka-ya-ardhi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/03/ridhiwani-kikwete-ataka-mipaka-ya-ardhi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy