Rais Samia Ataka Mabadiliko Taasisi Za Serikali
HomeHabari

Rais Samia Ataka Mabadiliko Taasisi Za Serikali

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa agizo la kufanywa mabadiliko katika Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kwe...


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa agizo la kufanywa mabadiliko katika Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kwenye ngazi zote za utendaji kazi.

Rais Samia ametoa agizo hilo jana wakati wa hafla ya kupokea Taarifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2020/2021 pamoja na Ripoti ya Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) Ikulu Chamwino, Dodoma.

Rais Samia amesema mabadiliko hayo ni kutokana na Bohari hiyo kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo hasa katika kuhudumia soko la nchi za Jumuiya ya Maendeleo za Kusini mwa Afrika (SADC).

Vile vile, Rais Samia ameagiza taasisi za Serikali zinazokopa mikopo chechefu kutoka Mifuko ya Hifadhi ya Jamii zirejeshe mikopo hiyo na kuwasilisha michango ya wafanyakazi katika mifuko hiyo.

Wakati huo huo, Rais Samia ameagiza kufanyike ukaguzi na tathmini ya mashirika ya umma na kuyafuta ambayo hayana tija kwa taifa. Mpaka sasa mashirika 38 yanaendeshwa bila Bodi ya Wakurugenzi.

Pia, Rais Samia ameitaka Ofisi ya Rais TAMISEMI kuzisisimamia Halmashauri ipasavyo pamoja na kuwachukulia hatua watumishi wenye matumizi mabaya ya fedha za Serikali.

Kwa upande mwingine, Rais Samia amaeipongeza TAKUKURU kwa kuweza kudhibiti matumizi mabaya ya fedha na kuitaka Taasisi hiyo kujiielekeza zaidi katika kuzuia kuliko kupambana na rushwa.

Hali kadhalika, amempongeza Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG ) kwa kuweza kupunguza kiwango cha hati chafu, na kuweza kudhibiti usimamizi wa rasilimali za umma.


Zuhura Yunus

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Rais Samia Ataka Mabadiliko Taasisi Za Serikali
Rais Samia Ataka Mabadiliko Taasisi Za Serikali
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj6hqPg4wYYbYyXMWJ-4CzwXEZLQFYk7EDyQWSU_fP7QqKUj58vynWEqJ7xpiHOj_c__HnlT_j7-kIEkp_4DtQII7fYW3SVFP32uI95pe1YJmuftr7uSX3U329_jcBIkp9WlxjH-gPlSYtPVwQA7W1RLQP0vGdIictKkOVjrDKRk4M-Ed-giBjVk7YFjQ/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj6hqPg4wYYbYyXMWJ-4CzwXEZLQFYk7EDyQWSU_fP7QqKUj58vynWEqJ7xpiHOj_c__HnlT_j7-kIEkp_4DtQII7fYW3SVFP32uI95pe1YJmuftr7uSX3U329_jcBIkp9WlxjH-gPlSYtPVwQA7W1RLQP0vGdIictKkOVjrDKRk4M-Ed-giBjVk7YFjQ/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/03/rais-samia-ataka-mabadiliko-taasisi-za.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/03/rais-samia-ataka-mabadiliko-taasisi-za.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy