Waziri Mkuu apokea taarifa ya Mauaji ya Mtwara na Kilindi
HomeHabari

Waziri Mkuu apokea taarifa ya Mauaji ya Mtwara na Kilindi

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amepokea taarifa ya kamati maalum aliyoiunda kwa ajili ya kuchunguza mauaji katika Mkoa wa Mtwara na Wilaya y...

Watu 9 wamefariki katika ajali ya boti Zanzibar
Mataifa makubwa kinyuklia yaahidi kupunguza silaha za nyuklia
Rais wa Msumbiji na mke wake wamekutwa na corona


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amepokea taarifa ya kamati maalum aliyoiunda kwa ajili ya kuchunguza mauaji katika Mkoa wa Mtwara na Wilaya ya Kilindi, Tanga.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa hiyo jijini Dar es Salaam, Waziri Mkuu ameipongeza kamati hiyo kwa kazi kubwa waliyoifanya na kwa umakini mkubwa.

“Taarifa hii imeeleza kila kitu bayana kabisa, na haya ndio matarajio ya Serikali yetu kwamba mtumishi yeyote ndani ya Serikali lazima awajibike kwa weledi, uaminifu na uadilifu mkubwa, kwa kufanya hivyo shughuli za kuwahudumia wananchi zitakwenda vizuri sana”

Amesema kuwa baada ya kuipitia taarifa hiyo ataiwasilisha kwa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye ndiye aliyetoa maagizo ya kuundwa kwa kamati hiyo ya kuchunguza mauaji kwenye Mikoa ya Mtwara na Tanga.

“Rais Samia anahitaji kuona matokeo, tena matokeo yasiyomuonea mtu yeyote, lakini matokeo yatakayomuwajibisha yeyote ambaye atagundulika kuhusika kutaka kuleta tafrani ndani ya nchi”

Kamati hiyo ilianza kazi Februari 4, 2022 ilipaswa kukamilisha ripoti yake ndani ya siku 14, zilizoishia Februari 17, 2022, lakini kutokana na ukubwa wa kazi na mahitaji ya kujiridhisha na baadhi ya masuala, kamati iliomba kuongezewa siku saba kuanzia Februari 17 hadi Februari 23, 2022.

Kamati hiyo iliundwa na Waziri Mkuu ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais Samia Suluhu Hassan alilolitoa Februari 4, 2022 Wilayani Magu, Mwanza akiwa njiani kuelekea Musoma, Mara kwenye maadhimisho ya miaka 45 ya CCM.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri Mkuu apokea taarifa ya Mauaji ya Mtwara na Kilindi
Waziri Mkuu apokea taarifa ya Mauaji ya Mtwara na Kilindi
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjOkHaDW3yd5AXHB_EKQWtF3zxBwHN8UJfoIzuxSfaP7Ym73vXQBjUOzmRHE69ADBPNvNFDvQeRneZgTG5gZCin9nYpV9FEI5bd3iH5cUd_5NdaxqPaOtWEgqyxNLOUrmVOnHmRDSRzywVUDw_SbP4UAozQmPU8Jg5fKo7HHMoSg8BJum6QQkd9-I6hQQ=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjOkHaDW3yd5AXHB_EKQWtF3zxBwHN8UJfoIzuxSfaP7Ym73vXQBjUOzmRHE69ADBPNvNFDvQeRneZgTG5gZCin9nYpV9FEI5bd3iH5cUd_5NdaxqPaOtWEgqyxNLOUrmVOnHmRDSRzywVUDw_SbP4UAozQmPU8Jg5fKo7HHMoSg8BJum6QQkd9-I6hQQ=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/waziri-mkuu-apokea-taarifa-ya-mauaji-ya.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/waziri-mkuu-apokea-taarifa-ya-mauaji-ya.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy