Taarifa Kwa Umma Kutoka Jeshi La Polisi Mbeya Kuhusu Tukio La Mauaji
HomeHabari

Taarifa Kwa Umma Kutoka Jeshi La Polisi Mbeya Kuhusu Tukio La Mauaji

 Mnamo tarehe 31/01/2022 majira ya saa 04:30 alfajiri huko Mtaa wa Hasanga uliopo Kata ya Uyole Tarafa ya Iyunga Jijini Mbeya, mtu mmoja ...


 Mnamo tarehe 31/01/2022 majira ya saa 04:30 alfajiri huko Mtaa wa Hasanga uliopo Kata ya Uyole Tarafa ya Iyunga Jijini Mbeya, mtu mmoja aitwaye JUSTIN NAMWINGA [55] Mwenyekiti wa Mtaa wa Hasanga alikutwa akiwa ameuawa kwa kuchomwa kisu kifuani chini ya titi la upande wa kushoto jirani na nyumbani kwake.

Awali kabla ya tukio hilo, JUSTIN NAMWINGA [55] alikuwa amelala na familia yake nyumbani kwake, walifika watu na kubisha hodi na kumjulisha kuwa kuna wezi nje, hivyo alitoka ili kutoa msaada baada ya muda kidogo majirani nao waliamka baada ya kusikia vishindo lakini walipofika nje walimkuta marehemu amelala kifudifudi huku akitokwa damu nyingi kifuani.

Chanzo cha tukio ni mapambano na wezi. Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya kwa uchunguzi wa kitabibu. Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na msako mkali kuwabaini na kuwakamata watuhumiwa wa tukio hili.

Aidha ninatoa rai kwa wananchi na yeyote mwenye taarifa za mtu/watu au kikundi cha watu waliohusika kwenye tukio hili watoe taarifa kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya ili watuhumiwa wakamatwe na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Imetolewa na:

[CHRISTINA A. MUSYANI – ACP]

KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Taarifa Kwa Umma Kutoka Jeshi La Polisi Mbeya Kuhusu Tukio La Mauaji
Taarifa Kwa Umma Kutoka Jeshi La Polisi Mbeya Kuhusu Tukio La Mauaji
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgC2jZUOFkO2JYzM4fVBjXJZpJauPRc_xkUe0WUeSa0n253OgVPG5CFrbrOiZWUAmNgmq_nmD3phqE-VWB2WC8F3IAqv47QTMUl1tq5_iBQ1abIXiOqsPhJdaW2seovG0nwx4P5whFTH6Ic46W-VsR0oAKYxgjfpsa0PpmKuqoGSzTySNq_98sMAR70pg=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgC2jZUOFkO2JYzM4fVBjXJZpJauPRc_xkUe0WUeSa0n253OgVPG5CFrbrOiZWUAmNgmq_nmD3phqE-VWB2WC8F3IAqv47QTMUl1tq5_iBQ1abIXiOqsPhJdaW2seovG0nwx4P5whFTH6Ic46W-VsR0oAKYxgjfpsa0PpmKuqoGSzTySNq_98sMAR70pg=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/taarifa-kwa-umma-kutoka-jeshi-la-polisi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/taarifa-kwa-umma-kutoka-jeshi-la-polisi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy