Rais Samia awaweka Kikaangoni RC, ma-DC, DED Mkoa wa Mara
HomeHabari

Rais Samia awaweka Kikaangoni RC, ma-DC, DED Mkoa wa Mara

Rais Samia Suluhu Hassan amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Mara (RC), Ally Hapi pamoja na wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri za mkoa hu...

Wizara Ya Afya Yaachana Na Mkandarasi Jengo La Mama Na Mtoto Geita
Mbarawa: Siku Zahesabika Kwa Wasimamizi Wa Mizani
Tangazo la Nafasi Mpya za Kazi Serikalini; LATRA, STAMICO, MUHIMBILI, TRC- ( Nafasi 353)


Rais Samia Suluhu Hassan amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Mara (RC), Ally Hapi pamoja na wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri za mkoa huo kijitathmini kama wanafaa kuendelea na nyadhifa zao.

Pia, ameagiza watu waliohusika na ujenzi wa mradi wa makao makuu ya halmashauri ya wilaya ya Bunda vijijini kukaa pembeni kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazowakabili ikiwemo rushwa hali iliyopelekea kukwama kwa mradi huo licha ya Sh400 milioni kutolewa kwaajili ya mradi huo.

Rais Samia ametoa maagizo hayo mjini Musoma  Jumapili Februari 6, 2022 baada kupokea taarifa mbalimbali juu ya kukwama kwa miradi ya maendeleo mkoa wa Mara tatizo ambalo amesema kuwa ni sugu.

Amesema kuwa inasikitisha kuona kuwa miradi mingi ya maendeleo inashindwa kukamilika kwa wakati huku kukiwa na uongozi kuanzia ngazi ya mkoa hadi wilaya hali ambayo inaonyesha kuwa viongozi hao wameshindwa kutimiza wajibu wao.

"Mkuu wa mkoa ni kama uliota maana leo nilikuwa nimepanga nikufyatue hapahapa bahati yako umeeleza matatizo haya ya kukwama kwa maendeleo ina maana unafanya kazi na matatizo haya unayajua na umenoyesha umechukua hatua gani una bahati" amesema Rais Samia

Amesema kuwa matatizo ya kukwama kwa maendeleo ya mkoa wa Mara yanasababishwa na viongozi waliopo Mara ambao amedai kuwa ni wabinafsi na wabadhirifu hivyo hataweza kumvumulia kiongozi yeyote anayekwamisha maendeleo.

Mbali na kuwataka viongozi hao kujitathmini lakini amesema kuwa suala la utendaji kazi wa viongozi hao anakwenda kulifanyia kazi na maamuzi atayatoa baada ya watu wake kufanya uchunguzi.

Kuhusu wakurugenzi wa halmashauri nchini Rais Samia amesema kuwa wakurugenzi hao walipewa muda wa matazamio ambao unaisha Februari 18 mwaka huu na kwamba tayari amemuagiza Waziri wa Tamisemi kumpa taarifa ya kila mkurugenzi ili aweze kufanya uchambuzi wa nani anabaki na nani anaondoka.

Amemuagiza RC Hapi kuvunja mikataba ya makandarasi wanaojenga miradi ya barababara za Makutano Sanzte yenye urefu wa kilomita 50 kwa gharama ya zaidi ya Sh60 bilioni pamoja na wa barabara ya Musoma Makojo yenye urefu wa kilomita 5 kwa gharama ya Sh8 bilioni.

Amesema kuwa umefika muda sasa miradi ya barabara itolewe kwa makandarasi wenye uwezo kuliko ilivyo sasa ambapo miradi hiyo ya barabara mkoani Mara imechelewa kwa sababu kadhaa ikiwemo uwezo mdogo wa makandarasi ki fedha na vifaa.

Rais Samia amefikia mamauzi hayo baada ya miradi hiyo kushindwa kukamilka wakati ambayo ni barabara ya Makutano Sanzate ilitakiwa kukamilika mwaka 2015 huku barabara ya Musoma mokojo ilikuwa ikitakiwa kukamilika mwezi Julai mwaka jana.

Kuhusu ombi la Mkuu wa Mkoa wa Mara la kufumua halmashuriza mkoa huo, Raais Samia amesema kuwa suala hilo lazima lifanyiwe kazi kwani serikali haiwezi kuwang'ang'ania watu wanaokwamisha maendeleo.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Rais Samia awaweka Kikaangoni RC, ma-DC, DED Mkoa wa Mara
Rais Samia awaweka Kikaangoni RC, ma-DC, DED Mkoa wa Mara
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiwcYeOB-v9H5X0jTnMiNrL1YQA7p1m9J5Y_R8mTqHjmER_UK8NX_fqIfw3KbMuzuPrmPvwWsSwZDTVYPGmxS-hQL-1VqGf_R58Ncqe1Tkij_Qsh6eYxY3b9C1DjopY2b2Eja2z1s2KAw_d6UYpPyDja7nWwAiEv8tL-G0Oo2owYwKJ1bMyY_1ymmFG6A=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiwcYeOB-v9H5X0jTnMiNrL1YQA7p1m9J5Y_R8mTqHjmER_UK8NX_fqIfw3KbMuzuPrmPvwWsSwZDTVYPGmxS-hQL-1VqGf_R58Ncqe1Tkij_Qsh6eYxY3b9C1DjopY2b2Eja2z1s2KAw_d6UYpPyDja7nWwAiEv8tL-G0Oo2owYwKJ1bMyY_1ymmFG6A=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/rais-samia-awaweka-kikaangoni-rc-ma-dc.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/rais-samia-awaweka-kikaangoni-rc-ma-dc.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy