Putin, Macron na Zelensky wajadili mgogoro wa eneo la mashariki ya Ukraine
HomeHabari

Putin, Macron na Zelensky wajadili mgogoro wa eneo la mashariki ya Ukraine

Ikulu ya rais wa Ufaransa ya Élysée imetangaza kuwa, baada ya kuzungumza na Rais Vladimir Putin wa Russia, rais wa nchi hiyo Emmanuel Mac...


Ikulu ya rais wa Ufaransa ya Élysée imetangaza kuwa, baada ya kuzungumza na Rais Vladimir Putin wa Russia, rais wa nchi hiyo Emmanuel Macron amezungumza kwa njia ya simu pia na mwenzake wa Ukraine Volodymyr Zelensky kumjulisha kuhusu mazungumzo yao.

Mazungumzo ya Macron, ambaye ni mwenyekiti wa sasa wa Umoja wa Ulaya na Putin yameonekana kutoa fursa ya mwisho ya kuuhitimisha mzozo wa Ukraine kwa njia za kidiplomasia, huku ikiripotiwa kuwa ukiukaji wa usitishaji mapigano katika eneo la Donbas mashariki ya Ukraine unaendelea kuongezeka.

Ofisi ya rais wa Ufaransa imeeleza katika taarifa kuwa, mazungumzo ya simu kati ya Rais Emmanuel Macron wa nchi hiyo na rais Vladimir Putin wa Russia yalidumu kwa muda wa saa 1:45.
Putin (kulia) na Macron

Kwa mujibu wa Ikulu ya Russia, Kremlin, katika mazungumzo aliyofanya kwa njia ya simu na rais wa Ufaransa hapo jana, Putin ametaka shirika la kijeshi la NATO na Marekani "zichukulie kwa uzito" madai ya nchi yake kuhusu usalama wake, ambao ndio kiini cha mzozo wa sasa kati ya Moscow na nchi za Magharibi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu ya Élysée, katika mazungumzo hayo ya jana Marais wa Ufaransa Emmanuel Macron na Vladimir Putin wa Urusi wamekubaliana pia kufanya kila linalowezekana ili kufikiwa haraka usitishaji mapigano mashariki mwa Ukraine



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Putin, Macron na Zelensky wajadili mgogoro wa eneo la mashariki ya Ukraine
Putin, Macron na Zelensky wajadili mgogoro wa eneo la mashariki ya Ukraine
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEg_PoEgbc-fvBJVPux-eNDOaLTVk0c_Jx8pVaCUrFf9kADUwoyUUUPgQkRMAJnOZ1msL62o-DhudbdcXu0QQi3hkLumUiMaEEC4kLbfvO7S2g81sd4gjDo2JMudJ1bfWYb3ZEjvW5LbHNJsWVuIlj2XkEIwy_fMIK4IlMSioEof4hSYHmz51aYrqx9aiw=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEg_PoEgbc-fvBJVPux-eNDOaLTVk0c_Jx8pVaCUrFf9kADUwoyUUUPgQkRMAJnOZ1msL62o-DhudbdcXu0QQi3hkLumUiMaEEC4kLbfvO7S2g81sd4gjDo2JMudJ1bfWYb3ZEjvW5LbHNJsWVuIlj2XkEIwy_fMIK4IlMSioEof4hSYHmz51aYrqx9aiw=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/putin-macron-na-zelensky-wajadili.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/putin-macron-na-zelensky-wajadili.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy