Dk.Mpango Atoa Pole Msibani Kwa Malecela
HomeHabari

Dk.Mpango Atoa Pole Msibani Kwa Malecela

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango akiongozana na mkewe Mama Mbonimpaye Mpango leo tarehe 20 Februari 2...


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango akiongozana na mkewe Mama Mbonimpaye Mpango leo tarehe 20 Februari 2022 wamefika nyumbani kwa Waziri Mkuu Mstaafu Samwel Malecela Mtaa wa Kilimani Jijini Dodoma  kutoa pole kufuatia kifo cha mtoto wake Dkt. Mwele Ntuli Malecela kilichotokea tarehe 10 Februari 2022 Geneva nchini Uswisi.

Akitoa neno la faraja kwa familia na waombolezaji mbalimbali waliojitokeza nyumbani hapo, Makamu wa Rais amewasihi kuwa na moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu pamoja na kumuombea marehemu apate pumziko la Amani.

Makamu wa Rais amemtaja Dkt. Mwele kama shujaa aliejitoa kupigania Afya za wananchi wengine kupitia tafiti mbalimbali alizokuwa akizifanya zenye lengo la kusaidia jamii kupambana na magonjwa mbalimbali. Amesema Dkt. Mwele alifanya kazi iliyo njema na kuonekana katika jamii ndani na nje ya nchi.

Aidha Makamu wa Rais amesema katika kipindi cha uhai wake Dkt. Mwele Malecela aliinua jina la Tanzania kwa kuaminiwa kufanya kazi katika taasisi kubwa ya afya duniani. Amesema uwezo wa Dkt. Mwele katika kazi pia uliinua wanawake hapa nchini hivyo hapana budi kumshukuru Mungu kwa zawadi hiyo pamoja kumuombea ampokee ili apumzike kwa Amani.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Dk.Mpango Atoa Pole Msibani Kwa Malecela
Dk.Mpango Atoa Pole Msibani Kwa Malecela
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgOcvQBzVgm4xppZLAUCUQyzD2P6ExAOAqz0lpOpC3m7-dL5bwS9T5U4yMOpbJPedEXZ0oeGxPRjhTzIVOkQjv80LXAiXRCJ7ldJHpIDIBufkkcO272md8lHW-p76MROrJXdQ8T0im0uf6QYIBXOozPWKqVOycxO_TWG7M_W5BnaIplvZ3hq7PqzJfICA=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgOcvQBzVgm4xppZLAUCUQyzD2P6ExAOAqz0lpOpC3m7-dL5bwS9T5U4yMOpbJPedEXZ0oeGxPRjhTzIVOkQjv80LXAiXRCJ7ldJHpIDIBufkkcO272md8lHW-p76MROrJXdQ8T0im0uf6QYIBXOozPWKqVOycxO_TWG7M_W5BnaIplvZ3hq7PqzJfICA=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/dkmpango-atoa-pole-msibani-kwa-malecela.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/dkmpango-atoa-pole-msibani-kwa-malecela.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy