Majaliwa: Tanzania Iko Mikononi Mwa Mungu
HomeHabari

Majaliwa: Tanzania Iko Mikononi Mwa Mungu

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania iko mikononi mwa Mungu na ndiyo maana imeendelea kuwa nchi yenye amani na utulivu na kimbili...

Rais Samia Afanya Uteuzi wa Kiongozi Mmoja
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo February 27
Waziri Mkuu apokea taarifa ya Mauaji ya Mtwara na Kilindi


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania iko mikononi mwa Mungu na ndiyo maana imeendelea kuwa nchi yenye amani na utulivu na kimbilio la mataifa yaliyopoteza tumaini.

“Nchi hii imeshikwa na Mwenyezi Mungu na ni kwa sababu viongozi wa dini wanaendelea kuliombea Taifa hili, kwa hiyo na sisi tunalo jukumu la kuhakikisha kwamba nchi hii inabaki kwa salama,” amesema.

Ametoa kauli hiyo  Ijumaa, Desemba 31, 2021 wakati akizungumza na waumini baada ya kushiriki ibada ya Ijumaa na kuzindua msikiti wa Nkowe, ulioko kata ya Nkowe, wilayani Ruangwa, mkoani Lindi.

Amesema Serikali zote tangu awamu ya kwanza hadi ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, zimeendeela kuheshimu uwepo wa dini nchini kwani miongozo na mafundisho yanayotolewa na viongozi wa dini mbalimbali yanawafanya waumini wao kuwa rai wema.

“Mheshimiwa Rais alipoingia madarakani alikutana na Mababa Askofu wote wa nchi hii, lakini pia alikutana na masheikh wote kupitia BAKWATA ili kupata miongozo na baraka za kuongoza nchi hii.”

Waziri Mkuu amewataka Watanzania wampe nafasi Rais Samia ya kufanya kazi kwa sababu amekuwa Serikalini kwa muda mrefu na anajua ni nini Watanzania wanatamani Serikali yao iwafanyie.

 Wakati huohuo, Waziri Mkuu amesema madaraka yote yanatoka kwa Mwenyezi Mungu na yeye ndiye hupanga nani awe nani na kwa wakati gani. “Tuache tabia ya kuwafanya viongozi washindwe kufanya kazi zao kwa kuwatengenezea migogoro ya kila siku, tena mengine ya kusingizia tu.”

“Kila nafasi imetengenezwa na Mwenyezi Mungu na kila anayekwenda kuongoza Mwenyezi ndiye amesema wewe utakuwa pale. Na kama hajasema, hutokuwa; utatumia hela nyingi na zitapotea bure. Utakwenda na mambo mengine ya giza, lakini hutomudu. Mwenyezi Mungu keshasema huyu ni huyu, tuwaheshimu walioko kwenye nafasi za kuwatumikia Watanzania wafanye kazi zao kwa weledi.”

Akizungumzia juhudi zinazofanywa na Serikali, Waziri Mkuu amesema hivi karibuni Serikali imetoa sh. bilioni 2.3 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa na vituo vya afya wilayani Ruangwa. Amesema wilaya hiyo ina uhakika wa kuwapeleka shule kwa wakati watoto wote waliofaulu kuingia kidato cha kwanza kwani madarasa yapo ya kutosha.

Waziri Mkuu yuko jimboni kwake Ruangwa kwa mapumziko ya mwisho wa mwaka.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Majaliwa: Tanzania Iko Mikononi Mwa Mungu
Majaliwa: Tanzania Iko Mikononi Mwa Mungu
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjEb_qPeIna5jCWQfi3XRshLL0fZ32Xx7AEqzV6gvNQ4ZOWRG9Cos739ykJDue8fG9TeIxfTkrS3qJcMyKNI7S7GlBJRgs7-rzftvpMcGgu3V2sVUSacLkSVy7szNGcW0gu4udzxKTVI9E3A_VeEyoCbOdgJyjjxlXLUP2iwjt-2MMbzGVOcQu6YP6kbA=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjEb_qPeIna5jCWQfi3XRshLL0fZ32Xx7AEqzV6gvNQ4ZOWRG9Cos739ykJDue8fG9TeIxfTkrS3qJcMyKNI7S7GlBJRgs7-rzftvpMcGgu3V2sVUSacLkSVy7szNGcW0gu4udzxKTVI9E3A_VeEyoCbOdgJyjjxlXLUP2iwjt-2MMbzGVOcQu6YP6kbA=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/01/majaliwa-tanzania-iko-mikononi-mwa-mungu.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/01/majaliwa-tanzania-iko-mikononi-mwa-mungu.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy