Waziri Mchengerwa Awataka Viongozi Kutozuia Likizo Za Watumishi Wa Umma
HomeHabari

Waziri Mchengerwa Awataka Viongozi Kutozuia Likizo Za Watumishi Wa Umma

Na. James K. Mwanamyoto-Geita Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa am...


Na. James K. Mwanamyoto-Geita

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema likizo ni haki ya mtumishi kisheria, hivyo hakuna haja ya Kiongozi kuzuia haki hiyo isipokuwa kwasababu maalum ambayo mtumishi husika atashirikishwa.

Mhe. Mchengerwa ameyasema hayo, wakati wa ziara yake ya kikazi ya kuhimiza uwajibikaji kwa Watumishi wa Umma na kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF Mkoani Geita.

Mhe. Mchengerwa amesisitiza kuwa, Kiongozi anapotaka kuzuia likizo ya mtumishi, afuate taratibu ambazo ni pamoja na kuzungumza na Mtumishi husika anayetaka kuchukua likizo aidha, kwa kumlipa gharama za kuzuia likizo hiyo au kumsogezea muda wa kuchukua likizo hiyo. 

Mhe. Mchengerwa amewataka Viongozi kuwa na utamaduni wa kusoma nyaraka mbalimbali za kiutumishi ili kujua sheria na taratibu zitakazowasaidia kuwaongoza pale wanapotaka kutoa matamko yanayozuia stahiki za mtumishi.

Mhe. Mchengerwa amefafanua kuwa, ni vizuri kuzungumza na mtumishi kwa kutumia lugha nzuri na akakuelewa kuliko kutumia cheo ulichonacho au lugha kali kwani unaweza ukazuia likizo yake na asifanye kazi inavyotakiwa.

“Sisi Viongozi tujitahidi sana kujenga matumaini kwenye mioyo ya watumishi tunaowaongoza, tuwasikilize na kutatua kero zao, tuwe karibu nao ili wasiwe waoga na hatimaye kupoteza ubunifu walio nao katika utendaji kazi wao,” Mhe. Mchengerwa amesisitiza.

Katika kusisitiza maelekezo yake, Mhe. Mchengerwa ameongeza kuwa, yeye ndiye Waziri anayesimamia masuala ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, hivyo ni lazima ahakikishe haki za watumishi zinapatikana kwani kama atashindwa kufanya hivyo, atakuwa hana sababu ya kuwepo kwenye wadhifa huo.

Mhe. Mchengerwa yuko kwenye ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Geita.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri Mchengerwa Awataka Viongozi Kutozuia Likizo Za Watumishi Wa Umma
Waziri Mchengerwa Awataka Viongozi Kutozuia Likizo Za Watumishi Wa Umma
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiCfxq0Ap5N5aWcS4GFLZpVfqmw_UltPGAJDxaVl1y0uk7z4V5Pej-MiSSnwshj7bXSsRkRU_jRHqrULCgelOYn_vzSbi7D-hTErZ7OFiUW9Cu7XGKAPMWt-Pv6gbK8u0Z578seN90RDIksrR3otGnWuCtItcjQalB0mXkjC42eo-QnpNXNTB_fzsj0gw=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiCfxq0Ap5N5aWcS4GFLZpVfqmw_UltPGAJDxaVl1y0uk7z4V5Pej-MiSSnwshj7bXSsRkRU_jRHqrULCgelOYn_vzSbi7D-hTErZ7OFiUW9Cu7XGKAPMWt-Pv6gbK8u0Z578seN90RDIksrR3otGnWuCtItcjQalB0mXkjC42eo-QnpNXNTB_fzsj0gw=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/waziri-mchengerwa-awataka-viongozi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/waziri-mchengerwa-awataka-viongozi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy