Wauza Madini Feki Wanaswa Sikonge
HomeHabari

Wauza Madini Feki Wanaswa Sikonge

  Na Lucas Raphael,Tabora Mwanamke mmoja mkazi wa mkoani wa Arusha amekamatwa na Jeshi la Polisi katika stendi ya mabasi wilayani Sikong...


 Na Lucas Raphael,Tabora
Mwanamke mmoja mkazi wa mkoani wa Arusha amekamatwa na Jeshi la Polisi katika stendi ya mabasi wilayani Sikonge Mkoani Tabora kwa tuhuma za kukutwa na madini feki aina ya Dhahabu  waliyokuwa wakiwauzia wananchi wa kishrikiana na dereva wake .

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari jana Kamanda wa Polisi Mkoani hapa ACP Richard Abwao alisema walimkamata Mariam Said, mkazi wa Arusha akiwa na dereva wake David George wakiwa na madini hayo waliyoyatumia kumtapeli mkazi wa kijiji cha Usunga wilayani humo aitwaye Edward.

Alibainisha kuwa watuhumiwa walikamatwa baada ya kumtapeli mkazi huyo kiasi cha sh 340,000 ambapo pia baada ya kukaguliwa walikutwa na kadi 5 za benki tofauti tofauti ambazo ni kadi za NMB 3, Posta 1na CRDB 1.

Vitu vinginevyo walivyokutwa navyo ni simu 4 aina ya iphone 6s plus, Tecno Spark 5 Air, Infinix hot 10 na Sam sung zinazodhaniwa kuwa za wizi.

Kamanda Abwao alibainisha kuwa madini hayo yamekamatwa kutokana na jitihada za Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na wananchi na vyombo vya ulinzi na usalama katika kuzuia, kutanzua na kupambana na uhalifu.

Aidha aliongeza kuwa katika kukabiliana na matukio ya uhalifu, mauaji, unyang’anyi wa kutumia silaha, ujambazi na uvunjaji Mkoani humo, Jeshi hilo limeendelea kufanya oparesheni mbalimbali katika wilaya zote.

Alitaja mafanikio ya oparesheni hiyo kwa mwezi huu kuwa ni kukamatwa watu 2 Khamis Baruti na Mohamed Shaban wakazi wa Izimbili wilayani Uyui kwa kukutwa na silaha aina ya gobore isiyo na namba za usajili iliyokuwa ikitumika kwenye uwindaji haramu.

Aidha walikamata silaha 2 aina gobore zilizosalimishwa na watu wasiojulikana katika kata za Kipanga na Mole ( Usanganya) wilayani Sikonge na silaha nyingine ilisalimishwa na mkazi wa Mibono John Matuzya katika Ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Kiloleni akidai anatii sheria bila shuruti.

Kamanda alitoa wito kwa wananchi wanazomiliki silaha kinyume na utaratibu kuendelea kuzisalimisha ndani ya kipindi hiki cha msamaha wa Waziri wa Ulinzi vinginevyo watakamatwa, aliitaka jamii kuendelea kushirikiana na Jeshi hilo kwa kutoa taarifa za vitendo vya uhalifu na wahalifu.


Mwisho.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Wauza Madini Feki Wanaswa Sikonge
Wauza Madini Feki Wanaswa Sikonge
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiwB0PdSyBtW3u_7XsH33TMom6KODQrUWD2RbB2mbyAuzsLeU6jHwqFhnjnHNZfNUp7GyU0VEeuGzX5MfM69M5DVYwMquwuc4KrwjERdrJK9itSlkfSvJwb4afvuV64qZBR9VaFRFl2fi274_esH5591LcWEijumhjybzTxHpnCwEngjNZ90DHMYYVN9Q=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiwB0PdSyBtW3u_7XsH33TMom6KODQrUWD2RbB2mbyAuzsLeU6jHwqFhnjnHNZfNUp7GyU0VEeuGzX5MfM69M5DVYwMquwuc4KrwjERdrJK9itSlkfSvJwb4afvuV64qZBR9VaFRFl2fi274_esH5591LcWEijumhjybzTxHpnCwEngjNZ90DHMYYVN9Q=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/wauza-madini-feki-wanaswa-sikonge.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/wauza-madini-feki-wanaswa-sikonge.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy