Majaliwa: Fedha Za Miradi Zitumike Kama Ilivyokusudiwa
HomeHabari

Majaliwa: Fedha Za Miradi Zitumike Kama Ilivyokusudiwa

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa miradi mbalimbali ya m...


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini ikiwemo wilaya ya Ruangwa, hivyo ni lazima fedha hizo zitumike kama ilivyokusudiwa.

Pia, Mheshimiwa Majaliwa ameagiza kwamba wenyeviti wote wa kamati za ujenzi wa mradi hiyo ikiwemo ya ujenzi wa vituo vya afya pamoja na shule watoke katika vijiji ambavyo miradi husika inatekelezwa ili kurahisisha usimamizi.

Ameyasema hayo leo (Jumatatu, Novemba 22, 2021) wakati akikagua ujenzi wa shule ya Sekondari Kitandi iliyoko Kata ya Likunja wilayani Ruangwa, Lindi akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua shughuli za maendeleo mkoani Lindi.

Waziri Mkuu amewataka watu wote walioko kwenye kamati zinaosimamia miradi hiyo  wawe waadilifu na wahakikishe wanadhibiti vitendo vya wizi katika maeneo yote yanayotekelezwa miradi na ijengwe kwa viwango. “Lazima tuzilinde fedha zilizotolewa na Rais wetu mpendwa.”

Amesema kuwa mpango wa Mheshimiwa Rais  Samia ni kuhakikisha watanzania wanapata huduma zote za kijamii ikiwemo Afya, maji, umeme, barabara ili kuwarahisishia kutekeleza shughuli zao “maendeleo haya yote ni kutokana na juhudi za mkuu wa nchi, lazima tumuunge mkono”

“Kiongozi wa nchi ametoa fedha, hatuwezi kuvumilia kuona mtu mzembe kwenye miradi ya Serikali, huu ni ujumbe kwa kamati zote zinazosimamia ujenzi wa miradi nchini. Wananchi wanatajaria kuona miradi hii inakamilika, simamieni miradi na iishe tena kwa viwango, Mheshimiwa Rais Samia anatoa fedha kwa ajili ya miradi hii ya wananchi”

Waziri Mkuu amesema kuwa wajumbe wote wa kamati za ujenzi wa miradi nchini washirikishwe kwenye hatua zote za ujenzi ikiwemo ununuzi wa vifaa vya ujenzi.

Kwa upande wake, Katibu wa Mradi huo Mwalimu Arafa Msuya amesema ujenzi wa shule hiyo mpya ya sekondari ya Kitandi ambayo ni ya bweni itakayosajili watoto wa kike na kiume kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita itapunguza adha ya wanafunzi wa maeneo hayo kutembea umbali mrefu hadi shule ya sekondari ya Likunja.

Alisema Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa imepokea shilingi bilioni moja kutoka Serikali Kuu kupitia mradi wa EP4R kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo unaojumuisha miundombinu ya majengo 16 ambayo ni jengo la utawala, majengo matano yenye jumla ya vyumba 13 vya madarasa.

Miundombinu mingine ni ujenzi wa mabweni manne yakiwemo mawili ya wanafunzi wa kike na mawili ya wanafunzi wa kiume, ujenzi wa nyumba mbili za walimu ambazo ni kila mmoja inauwezo wa kuishi familia mbili, ujenzi wa bwala la chakula na jiko la nje, matundu 30 ya vyoo na ujenzi wa kichomea taka.

Nao, mafundi wanaojenga mradi huo kupitia mfumo wa force account wameishukuru Serikali kwa kutoa fedha za ujenzi wa mradi huo kwa kuwa mbali na kusogeza huduma za jamii karibu na wakazi wa wananchi pia inatoa ajira kwa wananchi wengi hususani wanaoishi katika maeneo ya karibu. Wameahidi kuikamilisha kwa wakati na kwa viwango.


 (Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Majaliwa: Fedha Za Miradi Zitumike Kama Ilivyokusudiwa
Majaliwa: Fedha Za Miradi Zitumike Kama Ilivyokusudiwa
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhpvswC4yYYwols7nohPOgY8Yo7n5qhWb880mwbGqS0PJZUvVAPKEhl3a-1swZAGG_Ls7uzse4tWK7X_xhagjbkI6fULo9BN4hSNs8Kqqy0COutk31IUzChjeyGJgX0t84IX7pi2z--RVz6jCPhW-piPSH2gQZOmSwANjJbNudF-54ICjQmgc_kRJHiTA=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhpvswC4yYYwols7nohPOgY8Yo7n5qhWb880mwbGqS0PJZUvVAPKEhl3a-1swZAGG_Ls7uzse4tWK7X_xhagjbkI6fULo9BN4hSNs8Kqqy0COutk31IUzChjeyGJgX0t84IX7pi2z--RVz6jCPhW-piPSH2gQZOmSwANjJbNudF-54ICjQmgc_kRJHiTA=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/majaliwa-fedha-za-miradi-zitumike-kama.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/majaliwa-fedha-za-miradi-zitumike-kama.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy