Kesi ya kughushi cheti cha ndoa kuanza kusikilizwa Novemba 29
HomeHabari

Kesi ya kughushi cheti cha ndoa kuanza kusikilizwa Novemba 29

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa zaidi ya mara tano imeshindwa kuanza kusikilizwa kwa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka kati...


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa zaidi ya mara tano imeshindwa kuanza kusikilizwa kwa ushahidi wa mashahidi wa upande wa mashtaka katika kesi ya kughushi cheti cha ndoa inayomkabili Khairoon Jandu.

Hatua hiyo imekuja kufuatia wakili wa washtakiwa Abubakar Salim kutofika mahakamani na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kuliitisha jalada la kesi hiyo ofisini kwake.

Awali ilidaiwa kuwa upelelezi dhidi ya kesi hiyo ambayo inasikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Joseph Lwambano ulikwisha kamilika na mashahidi kuandaliwa kwa ajili ya kuanza kutoa ushahidi wao lakini imeahirishwa tena mpaka Novemba 29, mwaka huu ili kuangalia kama DPP atakuwa amerejesha jalada la kesi hiyo mahakamani hapo ama la.

Awali kesi hiyo ilipangwa kuanza kusikilizwa kwa mfululizo kuanzia Novemba Mosi /2 na 3/2021 ambapo mashahidi wa upande wa mashtaka walikwisha andaliwa na wakili wa serikali Ashura Mzava miongoni mwa mashahidi hao yumo Wakili wa kujitegemea Jerome Msemwa lakini ilishindikana baada ya DPP kuliitisha jalada la kesi hiyo.

Msemwa ambaye ni shahidi wa upande wa mashtaka alitarajiwa kuanza kutoa ushahidi wake kwenye kesi hiyo ya kughushi cheti cha ndoa inayomkabili Khairoon Jandu Novemba Mosi mwaka huu lakini alikwama kufuatia hatua hiyo ya kuitishwa kwa jalada.

Awali kabla ya jalada la kesi hiyo kuitishwa na DPP kesi hiyo ilikwama kuanza kusikilizwa kwa sababu wakili mshtakiwa, Abubakar Salim alikuwa na udhuru …Kwa mujibu wa taarifa iliyofikishwa mahakamani hapo wakili huyo alikwenda kuhudhuria kesi Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi.

Kufuatia taarifa hiyo,Wakili wa serikali Ashura Mzava alidai ni mara ya tano sasa kesi inashindwa kuanza kusikilizwa kwa sababu ya wakili wa utetezi kutofika mahakamani.

“Mheshimiwa hakimu pamoja na wakili kuleta taarifa hii lakini naona kuna mchezo anafanya hii ni mara ya tano sasa kesi inashindwa kuendelea kwa yeye kutofika mahakamani naandaa mashahidi lakini wakili haonekani mahakamani” alidai wakili Mzava.

Katika kesi hiyo Khairoon anadaiwa katika tarehe na mwezi usiofahamika mwaka 2020, jijini Dar es Salaam kwa njia ya udanganyifu alighushi cheti cha kuzaliwa cha mtoto Gurditsing Jandu, akionyesha kuwa kimetolewa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) wakati akijua kuwa ni uongo.

Katika shtaka lingine, Khairoon anadaiwa kuwa katika tarehe na mwezi usiofahamika mwaka 2020 alighushi cheti cha ndoa akionyesha kimetolewa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania Bakwata jambo alilojua kuwa sio kweli.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Kesi ya kughushi cheti cha ndoa kuanza kusikilizwa Novemba 29
Kesi ya kughushi cheti cha ndoa kuanza kusikilizwa Novemba 29
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEg3csbaEIKMHYxuxoS6-RZvjgbhZUJMrFLtyHO3wrlt6YWWu6QoWzlODZUcGjBDCb6WxpHxC_RhhXqS4J4dw7PRHW-3RE3QQOFI_8kymX1yfEM1IemtKpAWeBJUbfXdUngk69bb26d9GcC4eh083fCO58gOPyYfqzTKN1f3DvSmG8gpS6WC76Yf3y9tag=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEg3csbaEIKMHYxuxoS6-RZvjgbhZUJMrFLtyHO3wrlt6YWWu6QoWzlODZUcGjBDCb6WxpHxC_RhhXqS4J4dw7PRHW-3RE3QQOFI_8kymX1yfEM1IemtKpAWeBJUbfXdUngk69bb26d9GcC4eh083fCO58gOPyYfqzTKN1f3DvSmG8gpS6WC76Yf3y9tag=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/kesi-ya-kughushi-cheti-cha-ndoa-kuanza.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/kesi-ya-kughushi-cheti-cha-ndoa-kuanza.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy