Epukeni Vitendo Vya Rushwa Na Wizi Wa Dawa
HomeHabari

Epukeni Vitendo Vya Rushwa Na Wizi Wa Dawa

Na. WAMJW – Dar es Salaam Wafamasia nchini wametakiwa kusimamia miiko na maadili ya taaluma yao katika vituo vyao vya kazi na kuepuka vi...


Na. WAMJW – Dar es Salaam
Wafamasia nchini wametakiwa kusimamia miiko na maadili ya taaluma yao katika vituo vyao vya kazi na kuepuka vitendo viovu ikiwemo wizi wa dawa na ulaji rushwa.

Hayo yamesemwa jana na Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa Brig. Jen. Dkt. Gabriel Sauli Mhidize, alipo muwakilishai, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsi, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel Katika ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa Chama cha Fundi Dawa Sanifu na Fundi Dawa Wasaidizi (TAPHATA) uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Dkt. Mhidize kupitia ujumbe wa Naibu waziri wa Afya amesema, mkutano huo wa wana taaluma wote wa famasia wanatakuwa kuyafanyia kazi yote watakayo jifunza.

“Naamini mtaenda kufanya kazi kwa weledi wa hali ya juu kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za nchi katika kufikia lengo la utoaji wa huduma bora za Afya nchini” amesema Dkt. Mhidize

Kwa upande wake Msajili Baraza la Famasi, Elizabeth Shekalaghe ameiomba Serikali kupitia Wizara ya Afya iweke miongozo itakayotoa maelekezo kwenye sekta zote (binafsi na Serikali) kuwa na Wataalamu sahihi wa dawa katika ngazi za zahanati, vituo vya Afya na Hospitalini.

Bi.Shekalaghe amesema hatua hiyo itasaidia kuongeza Ajira kwa kada za wafamasia na zitasaidia kuboresha utoaji sahihi wa huduma bora za Afya nchini.

“Tukiwa tunaenda kwenye uchumi wa viwanda kwa kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, tunaomba viwanda vilivyopo nchini kuajili Wataalamu sahihi ili kuboresha uzalishaji wa dawa”amesema Shekalaghe.

Aidha, Bi.Shekalaghe ameiomba Wizara ya Afya kupitia taasisi zake kupitia upya viwango vya madaraja ya ufaulu wa kujiunga na vyuo vinavyotoa kozi ya Fundi Dawa Sanifu na Fundi Dawa Wasaidizi ili kupata Wataalamu sahihi na wenye uwezo wa kutoa huduma.

Mkutano huo utadumu kwa siku mbili kuanzia 29-30 mwezi wa 11, 2021 na umewashirikisha Wana taaluma wa ufamasia kutoka Tanzania Bara.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Epukeni Vitendo Vya Rushwa Na Wizi Wa Dawa
Epukeni Vitendo Vya Rushwa Na Wizi Wa Dawa
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiq4B6dxn4X-fes1XR8dztjni5Yd9YE2a7L7fEa-Ss2mzWFyIy2X7Uzrof1QoPkz67ojFueJJcrSnew3h6vZVqGl79svlH__ZtSl_zKqiII_cqEQVioDRzf-rH9LpC6vKmPLqnOg0yqTrvBxCnrW3mkJsd93xSxwvQxl9Ki9NcoFvW_quA_kH5AghTBrg=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiq4B6dxn4X-fes1XR8dztjni5Yd9YE2a7L7fEa-Ss2mzWFyIy2X7Uzrof1QoPkz67ojFueJJcrSnew3h6vZVqGl79svlH__ZtSl_zKqiII_cqEQVioDRzf-rH9LpC6vKmPLqnOg0yqTrvBxCnrW3mkJsd93xSxwvQxl9Ki9NcoFvW_quA_kH5AghTBrg=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/epukeni-vitendo-vya-rushwa-na-wizi-wa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/epukeni-vitendo-vya-rushwa-na-wizi-wa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy