Watanzania 7,713 Waajiriwa Mradi Wa Bwawa La Umeme Rufiji
HomeHabari

Watanzania 7,713 Waajiriwa Mradi Wa Bwawa La Umeme Rufiji

Na Ahmed Sagaff – MAELEZO Watanzania 7,713 wanafanya kazi kwenye Mradi wa Bwawa la Kufulia Umeme la Julius Nyerere (JNHPP) unaotekelezwa...


Na Ahmed Sagaff – MAELEZO
Watanzania 7,713 wanafanya kazi kwenye Mradi wa Bwawa la Kufulia Umeme la Julius Nyerere (JNHPP) unaotekelezwa wilayani Rufiji, Mkoa wa Pwani.
 

Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa ameyasema hayo leo jijini Mwanza alipokuwa akieleza kazi zinazofanywa na Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan.

 

“Wafanyakazi 7,713 ambao ni sawa na asilimia 89 ya wafanyakazi wote 8,635 waliopo katika mradi huu ni Watanzania,” ameeleza Msigwa.
 

Sambamba na hilo, amefahamisha kuwa wakandarasi wanaotekeleza mradi huu wameshalipwa shilingi trilioni 2.832 ambayo ni sawa na asilimia 35.62 ya fedha zote shilingi trilioni sita na bilioni 558 zitakazotumika kugharimia ujenzi huu.
 

“Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango yeye wiki hii amefanya ziara katika mradi wa ujenzi wa Bwawa la Umeme la Julius Nyerere katika mto Rufiji na kujionea kazi kubwa inayofanywa katika mradi huu,” amedokeza Msigwa.
 

Pamoja na hayo, Msemaji huyo amehabarisha kwamba mradi huu umebuniwa na kusanifiwa na Watanzania, na kwamba unasimamiwa na wahandisi wa Tanzania kupitia kitengo kilicho chini ya TANROADS kiitwacho TECU na unatekelezwa kwa fedha za Watanzania.
 

“Malighafi zinazotumika hususan tani 850,000 za saruji, tani 70,000 za nondo, tani 250,000 za pozzolana na malighafi nyingine zinatoka hapa hapa nchini kwetu,” amebainisha Msigwa.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Watanzania 7,713 Waajiriwa Mradi Wa Bwawa La Umeme Rufiji
Watanzania 7,713 Waajiriwa Mradi Wa Bwawa La Umeme Rufiji
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhoQ9joytrbMFhdK4KxL8Jf-yL0SV9zJd5D---AjnYk2osUGTPux2KGGnkJKrnTGV_eb5t_TKR2iyxT1d2j8XUczVXNLWk7Kdrce-084iuHTWM_5DVB2eqR2Xc4Q92zRG5eh2AbIYdvGcAuPdvbmyFauFlyYf6gsqFoiwECA_V0GzA0CFO3lXUF3xoXxQ=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhoQ9joytrbMFhdK4KxL8Jf-yL0SV9zJd5D---AjnYk2osUGTPux2KGGnkJKrnTGV_eb5t_TKR2iyxT1d2j8XUczVXNLWk7Kdrce-084iuHTWM_5DVB2eqR2Xc4Q92zRG5eh2AbIYdvGcAuPdvbmyFauFlyYf6gsqFoiwECA_V0GzA0CFO3lXUF3xoXxQ=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/watanzania-7713-waajiriwa-mradi-wa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/watanzania-7713-waajiriwa-mradi-wa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy