Ufaransa Kukarabati Uwanja Wa Ndege “Terminal Two”
HomeHabari

Ufaransa Kukarabati Uwanja Wa Ndege “Terminal Two”

Na Mwandishi Wetu, Dar Tanzania na Ufaransa zimekubaliana kuendelea kushirikiana katika maeneo ya kimkakati ikiwemo Nishati, Elimu, Kili...


Na Mwandishi Wetu, Dar
Tanzania na Ufaransa zimekubaliana kuendelea kushirikiana katika maeneo ya kimkakati ikiwemo Nishati, Elimu, Kilimo na Miundombinu ambapo Ufaransa umekubali kukarabati Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ‘Terminal Two’ Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) ameyasema hayo wakati akizungumza na Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester leo alipowasili Jijini Dar es Salaam kwa ziara ya kikazi ya siku moja.   

Kumekuwa na Miradi ambayo Serikali ya Ufaransa kupitia Shirika lao la Maendeleo wamekuwa wakifadhili Miradi mbalimbali katika Sekta mbalimbali hapa nchini zikiwemo sekta za Nishati, Elimu, Kilimo na Miundombinu.

Mtakumbuka kuwa Ufaransa ndiyo waliojenga Uwanja wa Ndege wa “Termirnal Two” wa Julius Kambarage Nyerere sasa wanakuja na mradi wa kukarabati uwanja huo na kuufanya kuwa wa kisasa zaidi. Sasa hivi tu terminal three lakini terminal two imekuwa ikitumika na ndege zinazofanya safari zake za ndani hapa nchini……..mradi huu ni moja kati ya mradi mkubwa na utakamilika hivi karibuni.

Waziri wa Biashara za Kimataifa na Uwekezaji wa Ufaransa, Mhe. Franck Riester yupo nchini Tanzania kuzindua safari za Shirika la ndege la Ufaransa ‘Fance Airline’ kutoka Paris hadi Zanzibar ambapo mara ya mwisho kwa shirika hilo kufanya safari zake hapa nchini ilikuwa mwaka 1974.

Septemba 15, 2021 Balozi wa Ufaransa hapa nchini Mhe. Nabil Hajlaouvi alisema Serikali ya Ufaransa kupitia Shirika lake la ndege ‘Fance Airline’ inategemea kuanzisha safari mpya ya ndege kutoka Ufaransa moja kwa moja hadi Zanzibar kuanzia 19 Oktoba 2021.

Katika tukio jingine, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) ametoa salamu za rambirambi kufuatia kifo cha aliyewahi kuwa waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Colin Powell.

“Kwa kweli Serikali ya Tanzania tumeshtushwa sana na kifo chake………katika kipindi chake aliendeleza uhusiano wa Marekani na Mataifa mbalimbali, kwa kweli ni masikitiko makubwa tutamkumbuka daima,” Amesema Balozi Mulamula


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Ufaransa Kukarabati Uwanja Wa Ndege “Terminal Two”
Ufaransa Kukarabati Uwanja Wa Ndege “Terminal Two”
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhiM2VMaJ0GOrEFf1eeQhrnsXi6uEqOa8XWP2OXkOQ4J71LoreJOcAbn6o_O54p5m67cbwD5qNGw2XYPEQlZ0jkr4RKEC4IY4iWIZTws1OIHW2pMkzDFld20bmaqalfrNsxoyiKUTtZaCmVLewSv_y5QYeHHN6P97j3YYx-MaT6n-pPEtPpAdMBaPUtSw=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhiM2VMaJ0GOrEFf1eeQhrnsXi6uEqOa8XWP2OXkOQ4J71LoreJOcAbn6o_O54p5m67cbwD5qNGw2XYPEQlZ0jkr4RKEC4IY4iWIZTws1OIHW2pMkzDFld20bmaqalfrNsxoyiKUTtZaCmVLewSv_y5QYeHHN6P97j3YYx-MaT6n-pPEtPpAdMBaPUtSw=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/ufaransa-kukarabati-uwanja-wa-ndege.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/ufaransa-kukarabati-uwanja-wa-ndege.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy