Serikali Yaipa Mwanza Bilioni 344 Kutekeleza Miradi Ya Maendeleo
HomeHabari

Serikali Yaipa Mwanza Bilioni 344 Kutekeleza Miradi Ya Maendeleo

Na Ahmed Sagaff - MAELEZO Mkoa wa Mwanza umepokea shilingi Bilioni 344 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya wananchi katika kipi...


Na Ahmed Sagaff - MAELEZO
Mkoa wa Mwanza umepokea shilingi Bilioni 344 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya wananchi katika kipindi cha miezi sita ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan.
 

Hayo yameelezwa leo jijini Mwanza na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa alipokuwa akitoa taarifa ya kazi zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita.

 

Amesema kiasi hicho cha fedha kimeelekezwa kwenye utekelezaji wa miradi ya ujenzi (bilioni 219.1), sekta ya afya (bilioni 15.2), sekta ya elimu (bilioni 38.7), miundombinu ya barabara (bilioni 2.4), usambazaji wa umeme vijijini (bilioni 42.6), miradi ya maji (bilioni 20.4) na mradi wa kusaidia kaya masikini unaotekelezwa na TASAF (bilioni 5.6).
 

Pamoja na hilo, Msigwa amehabarisha kuwa fedha hizo zitaendeleza ujenzi wa Stendi za Nyamhongolo na Nyegezi, Soko la Kisasa la Mjini, Jengo la Abiria pale kwenye uwanja wa Ndege wa Mwanza,  ujenzi wa MV Mwanza yenye uwezo wa kubeba abiria 1,200 na tani 400 za mizigo, na Daraja la Kigongo – Busisi lenye urefu wa kilometa 3.2.
 

“Tumeleta shilingi Bilioni 8.3 kwa ajili ya kujenga hospitali tatu za Wilaya ya Sengerema, Kwimba na Misungwi, kumalizia hospitali mbili za Wilaya ya Buchosa na Ilemela, kujenga vituo vya afya vitano na zahanati 21 na kukarabati na kujenga vituo vya huduma 48, aidha tumeleta shilingi Bilioni 6.4 kwa ajili ya kununua dawa,” amefahamisha Msigwa.
 

Akifafanua kuhusu shilingi bilioni 38.7 zilizoelekezwa kwenye sekta ya elimu mkoani Mwanza, Msigwa ameeleza kuwa shilingi bilioni 11 zinaimarisha miundombinu ya elimu kwenye shule za msingi na sekondari huku shilingi bilioni nane zikigharamia mradi wa elimu bila malipo.
 

“Na tunatarajia kuleta shilingi bilioni 19.7 kwa ajili ya kujenga madarasa 985, hizi ni zile fedha za Mpango wa Ustawi wa Jamii tulizopata kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF),” amedokeza Msemaji Mkuu wa Serikali.  




Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Serikali Yaipa Mwanza Bilioni 344 Kutekeleza Miradi Ya Maendeleo
Serikali Yaipa Mwanza Bilioni 344 Kutekeleza Miradi Ya Maendeleo
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEg9_ambdhS0gnsLn-VwIMCiU7FzbYBn5lq2vS5CPIxgoNiSItmS1BuHZeSR2H5WOYQ_s6bljBBgoUbXTKD59oufJsAVGAJvPs5Br6GvOs-oPqfx6z6QnZ9zwL3v1hqt07XZh2Dc3D7789Vo7laNw2P7ebXSsx6Axyhg3A4C_q4y2mD09VZ8zggG9gcs2g=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEg9_ambdhS0gnsLn-VwIMCiU7FzbYBn5lq2vS5CPIxgoNiSItmS1BuHZeSR2H5WOYQ_s6bljBBgoUbXTKD59oufJsAVGAJvPs5Br6GvOs-oPqfx6z6QnZ9zwL3v1hqt07XZh2Dc3D7789Vo7laNw2P7ebXSsx6Axyhg3A4C_q4y2mD09VZ8zggG9gcs2g=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/serikali-yaipa-mwanza-bilioni-344.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/serikali-yaipa-mwanza-bilioni-344.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy