Serikali Imepanga Kufanya Maboresho Makubwa Bohari Ya Dawa (MSD)
HomeHabari

Serikali Imepanga Kufanya Maboresho Makubwa Bohari Ya Dawa (MSD)

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imepanga kufanya maboresho ya kiutendaji katika Bohari ya Dawa (MSD) ili kuhakikisha wananch...


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imepanga kufanya maboresho ya kiutendaji katika Bohari ya Dawa (MSD) ili kuhakikisha wananchi wanapokwenda kwenye vituo vya kutolea huduma za afya wanapata dawa.

Mheshimiwa Majaliwa amesema lengo la maboresho hayo ni kuhakikisha dhamira ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ya kufikisha dawa na vifaa tiba vinapatikana nchini kote inatimia.

Ameyasema hayo jana (Jumanne, Oktoba 5, 2021) wakati akizungumza na watumishi, madiwani na wananchi wa halmashairi ya Mtama mkoani Lindi akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika mkoa huo.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mtama, Dkt. Dismas Masulubu ambaye alisema walipeleka shilingi milioni 300 Bohari ya Dawa mwaka wa fedha uliopita kwa ajili ya ununuzi wa dawa lakini hadi sasa hawajapelekewa.

“…MSD inatakiwa ifanyiwe maboresho kwa sababu wanalipwa fedha kwa ajili ya dawa na vifaa lakini dawa hazipatikani kwa wakati. Dhamira ya Mheshimiwa Rais Samia ni kuhakikisha dawa zinapatikana katika maeneo yote ya kutolea huduma.”

Waziri Mkuu ameiagiza MSD ihakikishe inapeleka dawa katika maeneo yote kwa wakati pamoja na kulipa madeni yote dawa inayodaiwa na baadhi ya hospitali, vituo vya afya na zahati ili wananchi wapate huduma kama ilivyokusudiwa.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amesema Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ameweka mikakati madhubuti inayolenga kumaliza tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika maeneo yote nchini yakiwemo ya Halmashauri ya Mtama.

Amesema Serikali inaendelea kutekeleza kampeni ya Mheshimiwa Rais Samia ya kumtua mama ndoo kichwani ili kuhakikisha huduma hiyo inapatikana karibu na makazi yao lengo likiwa ni kuwawezesha wanawake na vijana kupata muda wa kushiriki katika shughuli za kijamii.

Waziri Mkuu amesema Serikali imeweka mikakati madhubuti yenye lengo la kumaliza tatizo la maji nchini, hivyo wananchi wawe na subira na waendelee kuiunga mkono Serikali yao kwa kuwa imedhamiria kuwahudumia.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Serikali Imepanga Kufanya Maboresho Makubwa Bohari Ya Dawa (MSD)
Serikali Imepanga Kufanya Maboresho Makubwa Bohari Ya Dawa (MSD)
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgIuhTeQC5vzhHqArBEtuvqldEbdT85VANSv33b7OCqhaqa16lZmkgp-ogZq6THSfmYTjFUhmREaht6nKiibWaIUpDzAb01L7o3Qy0MHskVpc5t4ja5j1kLS9rNE5zsC2giEIy-o7r3uIHY/s16000/1.jpeg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgIuhTeQC5vzhHqArBEtuvqldEbdT85VANSv33b7OCqhaqa16lZmkgp-ogZq6THSfmYTjFUhmREaht6nKiibWaIUpDzAb01L7o3Qy0MHskVpc5t4ja5j1kLS9rNE5zsC2giEIy-o7r3uIHY/s72-c/1.jpeg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/serikali-imepanga-kufanya-maboresho.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/serikali-imepanga-kufanya-maboresho.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy