MZUNGUKO WA KWANZA WAKUSANYA MABAO 10 BONGO
HomeMichezo

MZUNGUKO WA KWANZA WAKUSANYA MABAO 10 BONGO

  BAADA ya  Ligi Kuu Bara kuanza msimu wa 2021/22 kasi imekuwa kubwa kwa kila timu kupambana kusaka pointi tatu huku katika michezo iliyo...

 


BAADA ya  Ligi Kuu Bara kuanza msimu wa 2021/22 kasi imekuwa kubwa kwa kila timu kupambana kusaka pointi tatu huku katika michezo iliyoshuhudiwa kwenye viwanja vitatu tofauti, ni Uwanja wa Karume ulikamilisha dakika 90 bila timu kupata bao.

Mchezo huo ulikuwa ni wa kukata na shoka kwa wawakilishi wa kimataifa kukutana uwanjani ambapo ilikuwa ni Biashara United wenyeji wanaopeperusha bendera kwenye Kombe la Shirikisho pamoja na Simba wanaopeperusha bendera kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika na ulikamilika kwa ubao kusoma Biashara United 0-0 Simba.

Ni mabao 10 pekee yamekusanywa katika mzunguko wa kwanza ambapo kinara wa utupiaji kwa sasa ni Vitalis Mayanga na alifunga mabao yote mawili, Uwanja wa Karatu wakati timu yake ya Polisi Tanzania ikiwaadhibu KMC mabao 2-0 Uwanja wa Karatu.

Pia mchezo ambao ulishuhudia mabao mengi yakikusanywa ukiachana na ule kati ya Polisi Tanzania na KMC ni ule wa Namungo 2-0 Geita Gold Uwanja wa Ilulu Lindi ambapo nyota wa mchezo alikuwa ni Obrey Chirwa aliyetoa jumla ya pasi mbili za mabao.

Kwa upande wa waamuzi ni Rafaeil Ikambi aliyechezesha mchezo wa Polisi Tanzania na KMC alitoa jumla ya kadi tano za njano kwenye mchezo huo akimpoteza Emmanuel Mwandembwa ambaye alitoa kadi tatu kwenye mchezo wa Biashara United na Simba na pia huyu alishuhudia John Bocco akikosa penalti dakika za lala salama.


Imeandikwa na Dizo_Click



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: MZUNGUKO WA KWANZA WAKUSANYA MABAO 10 BONGO
MZUNGUKO WA KWANZA WAKUSANYA MABAO 10 BONGO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjOJ5lmFDdjHy72TBNXJJW-_oDiL6iJBKS8Uz_tTmNG-nAJmTifgHzlYyvD_fQOJ3H1AnAlEjoO6Q23Q7wOjp8OvP05sHalRL99wdk2Hhb8YhEdkha29VZRtahYhxTa17fBhL1ugJBv_5mf/w640-h640/officialmbeyakwanzafc-243476525_1057584394779753_9015032029836053727_n.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjOJ5lmFDdjHy72TBNXJJW-_oDiL6iJBKS8Uz_tTmNG-nAJmTifgHzlYyvD_fQOJ3H1AnAlEjoO6Q23Q7wOjp8OvP05sHalRL99wdk2Hhb8YhEdkha29VZRtahYhxTa17fBhL1ugJBv_5mf/s72-w640-c-h640/officialmbeyakwanzafc-243476525_1057584394779753_9015032029836053727_n.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/mzunguko-wa-kwanza-wakusanya-mabao-10.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/mzunguko-wa-kwanza-wakusanya-mabao-10.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy