Majaliwa: Rais Samia Amedhamiria Kuboresha Miundombinu
HomeHabari

Majaliwa: Rais Samia Amedhamiria Kuboresha Miundombinu

 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuboresha miundombinu ili Watanzania waendeshe shugh...


 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuboresha miundombinu ili Watanzania waendeshe shughuli zao kama za usafirishaji wa abiria na mizigo kwa urahisi na kukuza uchumi wa nchi na mtu mmoja mmoja.

“…endeleeni kutumia fursa za maendeleo zilizoletwa kupitia fedha za kodi katika kujipatia maendeleo na kukuza uchumi wenu kwani mna Serikali imara, Rais imara na wasaidizi wake wanafanya kazi usiku na mchana kwa ajili yenu.”

Ameyasema hayo jana (Jumatatu, Oktoba 25, 2021) baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa barabara ya Nanganga-Ruangwa (km 53.2) akiwa kwenye ziara ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali mkoani Lindi.

Baada ya kukagua ujenzi wa barabara hiyo unaosimamiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Waziri Mkuu aliuagiza uongozi wa wakala huo usimamie vizuri mradi huo na uhakikishe inajengwa kwa viwango.

“TANROADS simamieni vizuri ujenzi wa mradi huu na mhakikishe barabara inajengwa kwa viwango na inakamilika kwa wakati. Mliopata ajira katika mradi huu fanyeni kazi kwa weledi hatutarajii kusikia mtu ameiba nondo wala saruji.”

Barabara hiyo inajengwa na kampuni ya China Railway 15 Bureau Group Corporation ya China kwa gharama za shilingi bilioni 59.28 na imepangwa kukamilika Novemba 2022.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Mhandisi, Rogatus Hussein Mativila alisema hadi kufikia mwezi Septemba mwaka huu ujenzi wa barabara hiyo ulikuwa umefikia asilimia 32.

Mhandisi Mativila alitaja kazi zilizofanyika katika mradi huo kuwa ni pamoja na kusafisha eneo la ujenzi, ujenzi wa kitako cha barabara, uinuaji wa tuta kwenye maeneo ya mabonde, ukataji wa maeneo yenye miinuko mikubwa na ujenzi wa makalavati.

Kadhalika, Mtendaji Mkuu huyo alitaja barabara za mkoa wa Lindi ambazo Serikali imepanga kuzijenga kwa kiwango cha lami kuwa ni barabara ya Liwale-Nachingwea (km 130) ambayo ipo kwenye hatua ya kufanyiwa upembuzi yakinifu.

“Barabara ya Kiranjeranje-Namichiga-Ruangwa yenye urefu wa km 102 na barabara ya Masaninga-Nangukuru-Kilwa Masoko yenye urefu wa km 55 tayari zimeshafanyiwa tayari imeshanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina”

Akizungumzia kuhusu barabara ya Nangurukuru-Liwale Mhandisi Mativila alisema mkataba wa kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina tayari umeshasainiwa na kazi hiyo inatarajiwa kuanza ndani ya kipindi cha mwezi mmoja.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Majaliwa: Rais Samia Amedhamiria Kuboresha Miundombinu
Majaliwa: Rais Samia Amedhamiria Kuboresha Miundombinu
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgkM5VG4Hb3GlU4NHDPBayHMbHZSCnboet-uQig-jBqpd831dChon29wpszzIohN-YJTXctHRJg5TqwoWWhzXxyzBpEihKbZdmGVijXBOd-fQqAmgVEeBmMMbfY5lmPacSWCB8G9-rqSwgx2G0lWC5GjBbYSLpmh46jixe-6Hq4AahBsSiCk8la7T9NVA=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgkM5VG4Hb3GlU4NHDPBayHMbHZSCnboet-uQig-jBqpd831dChon29wpszzIohN-YJTXctHRJg5TqwoWWhzXxyzBpEihKbZdmGVijXBOd-fQqAmgVEeBmMMbfY5lmPacSWCB8G9-rqSwgx2G0lWC5GjBbYSLpmh46jixe-6Hq4AahBsSiCk8la7T9NVA=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/majaliwa-rais-samia-amedhamiria.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/majaliwa-rais-samia-amedhamiria.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy