Jeshi lachukua mamlaka kamili Sudan, hali ya hatari yatangazwa
HomeHabari

Jeshi lachukua mamlaka kamili Sudan, hali ya hatari yatangazwa

Jeshi la Sudan limevunja serikali ya mpito iliyokuwa inajumuisha raia na wanajeshi na wakati huo huo kuwakamata viongozi wa kisiasa akiwe...


Jeshi la Sudan limevunja serikali ya mpito iliyokuwa inajumuisha raia na wanajeshi na wakati huo huo kuwakamata viongozi wa kisiasa akiwemo waziri mkuu na kutangaza hali ya hatari nchi nzima.

Jenerali Abdel Fattah Burhan, ambaye alikuwa akiongoza baraza la pamoja na viongozi wa kiraia, ametoa tangaza hilo na kusema mapinduzi ya sasa ya kijeshi yamesbabaishwa na malumbano ya kisiasa.

Amedai kuwa jeshi limelazimika kulinda usalama wa nchi kwa mujibu wa katiba na kuongeza kuwa mbali na serikali ya mpito kuvunjwa  magavana wote wa majimbo nao wamefutwa kazi na kwamba uchaguzi utafanyika Julai 2023.

Kufuatia uamuzi huo wa jeshi, waandamanaji wenye hasira  wamemiminika  kwenye barabara za mji mkuu, Khartoum na kuwasha matairi barabarani huku milio ya risasi ikiendelea kusikika katika jiji hilo.

Viongozi wa jeshi na raia wamekuwa wakizozana tangu kiongozi wa muda mrefu Omar al-Bashir kupinduliwa miaka miwili iliyopita na serikali ya mpito kuanzishwa.

Waziri Mkuu Abdallah Hamdok ni miongoni mwa viongozi wa kiraia ambao wamezuiliwa nyumbani. Chama cha wanataaluma cha Sudan ambacho ni mwamvuli wa vyama vya wafanyakazi ambavyo vilikuwa muhimu katika maandamano ya mwaka 2019 ya kumpinga Bashir, kimeshutumu kile walichokiita "mapinduzi ya kijeshi" na kuwataka waandamanaji kupinga vikali hatua hiyo.

Ripoti zimebaini kuwa mawasiliano ya mtandao yamekatishwa na kwamba jeshi na vikosi vya kijeshi vimepelekwa kote jijini Khartoum. Aidha uwanja wa ndege wa Khartoum sasa umefungwa, na safari za ndege za kimataifa zimesimamishwa.




Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Jeshi lachukua mamlaka kamili Sudan, hali ya hatari yatangazwa
Jeshi lachukua mamlaka kamili Sudan, hali ya hatari yatangazwa
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiarABTS2NJPg2XcCRI9O8ORZOIS0otxdPnjaJNLH0l3pKoT5eJkH4nmmNmbwopokjuRGu_ajaf62yx0xvFta1denWHAFX-MeXCUeQY2fxTnehQYqQ_PXPboOXZRhezzmQHoV_nknAtpzZMOBp-yDQMjek1qRv9y5OmqxUG6vwtHoacK4gRXtQBDFfJUg=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiarABTS2NJPg2XcCRI9O8ORZOIS0otxdPnjaJNLH0l3pKoT5eJkH4nmmNmbwopokjuRGu_ajaf62yx0xvFta1denWHAFX-MeXCUeQY2fxTnehQYqQ_PXPboOXZRhezzmQHoV_nknAtpzZMOBp-yDQMjek1qRv9y5OmqxUG6vwtHoacK4gRXtQBDFfJUg=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/jeshi-lachukua-mamlaka-kamili-sudan.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/jeshi-lachukua-mamlaka-kamili-sudan.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy