Serikali Yapunguza Tozo Za Miamala Ya Simu
HomeHabari

Serikali Yapunguza Tozo Za Miamala Ya Simu

 Na Immaculate Makilika – MAELEZO  Serikali imefikia uamuzi wa kupunguza tozo za miamala ya simu kwa asilimia 30 kwa mtu anayetuma na kupo...

 Na Immaculate Makilika – MAELEZO
 Serikali imefikia uamuzi wa kupunguza tozo za miamala ya simu kwa asilimia 30 kwa mtu anayetuma na kupokea fedha za miamala kwa viwango vyovyote vinavyotumwa na kupokea, isipokuwa wale wanaotumia kati ya shilingi sifuri hadi shilingi 999.

  Sambamba na kampuni za simu kupunguza gharama za kutuma na kupokea fedha kutoka mtandao mmoja kwenda mtandao mwingine kwa asilimia 10, baada ya Serikali kujadiliana nao. Hivyo Serikali imetoa muda wa kati ya tarehe 01 Septemba hadi tarehe 07 Septemba, 2021 kwa kampuni hizo za simu kuweka sawa mitambo yao ili punguzo la asilimia 30 na asilimia 10 lianze.


 Hayo yamesemwa jana jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa wakati alipokuwa akizungunza na waandishi wa habari

  Msigwa alisema “Napenda kusisitiza kuwa tozo hizi zinakusanywa kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania. Kama ambavyo mmejulishwa katika kipindi cha mwezi mmoja na nusu tumekusanya jumla ya shilingi bilioni 63 (hadi tarehe 31 Agosti, 2021) na sasa fedha hizi zimepelekwa katika tarafa 150 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa vituo vya afya na tarafa nyingine 70 zitapelekewa fedha muda wowote kuanzia sasa kwa ajili ya kujenga Vituo vya Afya.”

 Aidha, amesema kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha wanafunzi wakakae vizuri madarasani badala ya kusoma kwenye magofu ama majengo yaliyoharibika, hivyo  fedha hizo pia zimepelekwa maeneo mbalimbali nchini kwa ajili ya kujenga na kumaliza maboma ya vyumba vya madarasa 560 kwa ajili ya wanafunzi ambao wataanza darasa la kwanza na kidato cha kwanza mwaka 2022.

 “Mwaka ujao 2022 tunatarajia kupokea wanafunzi 933,289 ambayo ni sawa na maoteo ya  asilimia 83.7 ya wanafunzi 1,115.041 waliosajiliwa kufanya mtihani wa darasa la saba ikilinganishwa na wanafunzi 833,872 tuliowapokea Januari mwaka huu 2021, sasa watoto wetu hawa wanahitaji vyumba vya madarasa na madawati” alisisitiza Msigwa



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Serikali Yapunguza Tozo Za Miamala Ya Simu
Serikali Yapunguza Tozo Za Miamala Ya Simu
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiY-RaBtlqM0GXbhyphenhyphenLBYBceezmoRISmXApbwKxnirLEgqM1uYEFZtb1tosO_VNS7JECSIqKIMgKL7pYqBnzXDy5Bacaz2Ik3Oq6lzqY_kJDTqHlo-GGT9-NMwt9ghLXc8FozO_eA5kJJLAW/s0/1.png
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiY-RaBtlqM0GXbhyphenhyphenLBYBceezmoRISmXApbwKxnirLEgqM1uYEFZtb1tosO_VNS7JECSIqKIMgKL7pYqBnzXDy5Bacaz2Ik3Oq6lzqY_kJDTqHlo-GGT9-NMwt9ghLXc8FozO_eA5kJJLAW/s72-c/1.png
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/09/serikali-yapunguza-tozo-za-miamala-ya.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/09/serikali-yapunguza-tozo-za-miamala-ya.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy