RC Tabora Atoa Angalizo Kwa Watoa Huduma Wa Chanjo
HomeHabari

RC Tabora Atoa Angalizo Kwa Watoa Huduma Wa Chanjo

NA TIGANYA  VINCENT MKUU wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt Batilda Buriani amewataka wafanyakaziwa sekta ya afya waliopewa jukumu ya kuendes...


NA TIGANYA  VINCENT
MKUU wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt Batilda Buriani amewataka wafanyakaziwa sekta ya afya waliopewa jukumu ya kuendesha zoezi la kutoa chanjo ya UVIKO 19 kuwa waadilifu na kufanyakazi kwa uzalendo.

Ametoa kauli hiyo leo wakati wa uzinduzi wa utoaji wa chanjo ya UVIKO kwa makundi mbalimbali iliyofanyika Kimkoa mjini Tabora.

“Naelekeza pia kwa huu mgao wa COVAX FACILITY ni marufuku Hospitali yoyote (ya umma au binafsi) kulipisha Wananchi gharama yoyote katika zoezi hili la chanjo na lifanyike kwa uadilifu na kwa haki kwa walengwa wa sasa” amesisitiza

Balozi Dkt Batilda Buriani amesema kuwa chanjo hiyo kwa sasa zinatolewa kwa kufuata vipaumbele vya makundi yenye uhitaji mkubwa ambayo ni Watumishi wa sekta ya Afya, watu wazima wenye umri wa miaka 50 na kuendelea na  watu wenye magonjwa sugu.

Amesema uchanjaji kwa makundi yote nchini ni wa hiari au huru kwa kila mwananchi.

Balozi Dkt, Batilda amesema Tabora imepata kiasi cha chanjo 30,000 ambazo zitatoa  fursa kwa Wananch ambao wako tayari kuchanjwa kupunguza kasi ya maambukizi ya ugonjwa wa COVID-19 pamoja na kupunguza hatari ya kupata ugonjwa na madhara makubwa endapo mtu atapata maambukizi.

Amesema kwa Mkoa wa Tabora umeanza rasmi utoaji wa chanjo ya UVIKO-19  tarehe 03 Agosti 2021 katika vituo vilivyoainishwa katika Mkoa ambavyo ni vituo vitatu (3) kwa kila Halmashauri na kufanya Mkoa wa Tabora kuwa na jumla ya vituo 24.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora (RMO) Dkt. Honoratha Rutatinisibwa amewataka watu waliochanja kuendelea kuchukua hatua za kujikinga na UVIKO 19.

Amesema katika nchi ambazo wamechanjwa wamepunguza vifo na kulaza wagonjwa.

Kwa upande wa Askofu wa Kanisa la Anglikana Dkt. Elias Chakupewa ameitaka jamii kuacha upotoshaji kuhusu chanjo badala yake waendelee kuwatia moyo wataalamu.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: RC Tabora Atoa Angalizo Kwa Watoa Huduma Wa Chanjo
RC Tabora Atoa Angalizo Kwa Watoa Huduma Wa Chanjo
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiPo4Uqmqj6JkVjoTNuZ7aXeGDD9p8wbb_Dmjd_-iTf4aerut8LyP-nojfx8DhMTnX6MG0Q2v5S9TAutoQGwQjqVs1TXp7xss_xBSM5VVESjbv25kSQvK8v74xCr_qRv2uDwgQa025ipIXP/s16000/2.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiPo4Uqmqj6JkVjoTNuZ7aXeGDD9p8wbb_Dmjd_-iTf4aerut8LyP-nojfx8DhMTnX6MG0Q2v5S9TAutoQGwQjqVs1TXp7xss_xBSM5VVESjbv25kSQvK8v74xCr_qRv2uDwgQa025ipIXP/s72-c/2.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/rc-tabora-atoa-angalizo-kwa-watoa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/rc-tabora-atoa-angalizo-kwa-watoa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy