MUDA WA KUANZA KUPATA HASIRA UPO KWENYE KONA KWA SASA
HomeMichezo

MUDA WA KUANZA KUPATA HASIRA UPO KWENYE KONA KWA SASA

  HESABU za usajili ndani ya ardhi ya Bongo zinatarajiwa kufungwa Agosti 31 baada ya kuwa na muda wa mwezi hivi katika purukushani za kusa...


 HESABU za usajili ndani ya ardhi ya Bongo zinatarajiwa kufungwa Agosti 31 baada ya kuwa na muda wa mwezi hivi katika purukushani za kusaka wachezaji wapya.

Kila kitu kwa sasa kwa asilimia kubwa kipo wazi kwani zipo timu ambazo zilifunga kabisa masuala ya usajili ikiwa ni pamoja na Azam FC, Biashara United hawa walimaliza shughuli mapema kabisa.

Wale ambao bado wapo sokoni ni muda wao wa kufunga hesabu kwani hakuna tena muda wa kuongeza. Taarifa rasmi kutoka Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF) iliweza kubainisha suala hilo.

Jambo la msingi kwa sasa kwa zile ambazo hazijakamilisha zipambane kufikia malengo kwani bila kufanya hivyo mambo yatakwenda mrama.

Muda ule ambao unasubiriwa kwa shauku kubwa na wadau ni ligi kuanza. Huo muda kwa sasa upo kwenye kona unakaribia kutua na mambo yataanza kuwa hewani kama kawaida.Wakati ule wa hasira kwa timu ambayo itakwama kufikia malengo na wachezaji ambao mambo yatakuwa magumu kwao.

Kama vile ambavyo ulianza usajili kwa kasi na ghafla kwa sasa ni siku tu inahesabiwa kisha mambo yanakuwa mengine ndivyo ambavyo itakuwa hivyo hata muda ue wa lawama utakavyofika.

Ikishachezwa mechi ya Ngao ya Jamii kati ya Simba na Yanga mambo yanakuwa yapo karibu. Ni muda wa kujua nani alipanda kwa wakati sahihi na nani alikurupuka kupanda.

Haina tabu kubwa sana kwenye kutambua nani aliweza kwenda na wakati kwa kuwa mavuno yake yanaonekana na ipo wazi kabisa.

Mavuno ya kile ambacho kimepandwa wakati wa usajili pamoja na maandalizi ya ligi kwa ujumla huwa yanapatikana ndani ya dakika 90 za ushindani.

Hapo kila mmoja anakwenda kujua maana halisi ya rangi ambayo ilikuwa imepambwa kama ni nyekundu ama nyeupe wakati ule wa usajili na maandalizi ya ligi kwa ujumla.

Ni muda wa kwenda kuwaona wale makipa ambao tumeambiwa kwamba wanadaka mpaka mishale wakiwa langoni.

Kazi ipo kwa kuwa kila mmoja anatamba kuwa na timu imara na bora. Basi kipimo cha ubora kinakuja na uthibitisho utapatikana.

Ipo wazi kabisa kwamba zipo timu ambazo zinakwenda kuanza kwa anguko katika mzunguko wa kwanza kwa sababu maandalizi yao yamekuwa ni ya kawaida.

Kwa hawa lazima wajipange mapema kwa kuanza kuangalia gia ambayo wataanza nayo na kuibadili mapema kabla ya mzunguko wa pili.

Mzunguko huu wa kwanza mara nyingi imekuwa kawaida timu kuuchukulia kama ni wa majaribio jambo ambalo huwa linakuja kuwagharimu baadaye hasa kwenye mzunguko wa pili.

Kwa timu ambayo imeweka malengo makubwa lazima hesabu zianze kufanya kazi wakati huu ili hata ule muda wa jioni utakapofika kila mmoja awe ana kitu cha kuanzia.

Sio inafika jioni katika mzunguko wa pili hapo watu wanaanza kutafuta pakutokea, itafahamika tu kama ilikuwa ni nyekundu ama nyeupe.

 



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: MUDA WA KUANZA KUPATA HASIRA UPO KWENYE KONA KWA SASA
MUDA WA KUANZA KUPATA HASIRA UPO KWENYE KONA KWA SASA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh_n5T2dwZt66IFzL31fYmzQcwp3PhthyphenhypheniErZNJaqcS1zJZZZZXTyuwj37NF623rZV1y8DqeioxGyicuWtVe5wbOxMdnR2_tuTScsJa325aEsECrkqtxz-CXLopiulHkqk-yuwfMWKPuSyw/w640-h622/237201790_837497647157640_2469709866150453903_n.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh_n5T2dwZt66IFzL31fYmzQcwp3PhthyphenhypheniErZNJaqcS1zJZZZZXTyuwj37NF623rZV1y8DqeioxGyicuWtVe5wbOxMdnR2_tuTScsJa325aEsECrkqtxz-CXLopiulHkqk-yuwfMWKPuSyw/s72-w640-c-h622/237201790_837497647157640_2469709866150453903_n.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/muda-wa-kuanza-kupata-hasira-upo-kwenye.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/muda-wa-kuanza-kupata-hasira-upo-kwenye.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy