Mawaziri Wa Fedha Tanzania Bara Na Zanzibar Kutatua Changamoto Za Miradi
HomeHabari

Mawaziri Wa Fedha Tanzania Bara Na Zanzibar Kutatua Changamoto Za Miradi

Na. Saidina Msangi na Sandra Charles, WFM, Dodoma Waziri wa Fedha na Mipango wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lamec...


Na. Saidina Msangi na Sandra Charles, WFM, Dodoma
Waziri wa Fedha na Mipango wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Jamal Kassim Ali, wamekubaliana kutatua changamoto za utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kufanya kazi kwa kushirikiana ili kukuza uchumi wa Taifa.

Mawaziri hao wamekutana jijini Dodoma katika kikao kazi kilicholenga kuangalia masuala yaliyokuwa na changamoto wakati wa bunge la bajeti na Sheria ya Bajeti pamoja na masuala yanayohusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Dkt. Nchemba alisema kuwa kikao hicho kimekuwa cha mafanikio ambapo mengi yamefikia hatua nzuri na kuongeza wigo wa ushirikishwaji hasa katika kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mipya ya kipaumbele iliyoko katika Bajeti Kuu ya Serikali.

“Katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo tunaangalia uwezeshaji na utekelezaji wa miradi inayoendelea na miradi mipya, na mengi tuliyojadili tumefikia hatua nzuri,” alisema Dkt. Nchemba.

Waziri Nchemba aliwaagiza wataalamu wa pande zote kuendelea kufanyia kazi maeneo ya changamoto yaliyosalia ikiwemo uboreshaji wa Sheria ya Usajili wa Vyombo vya Moto.

“Niwasihi msiishie kwenye Sheria ya Vyombo vya Moto ila muangalie na waendeshaji wa vyombo vya moto haipendezi mtu kuwa na leseni mbili wakati nchi ni moja”, alisisitiza Dkt. Nchemba.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Jamal Kassim Ali, alisema kuwa kikao kati yake na mwenzake Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba kimetoa njia ya namna ya kutatua changamoto mbalimbali za maendeleo hususani za miradi.

Alisema kuwa wamejadili namna ya kufanikisha upatikanaji wa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati iliyopo upande wa Zanzibar, jambo ambalo lina tija kwa wananchi wa Zanzibar.

“Hili ni jambo muhimu tunashukuru uwepo wa kikao hiki ambacho kinatoa mwanga wa namna miradi ya kimkakati Zanzibar itatekelezwa na uwezeshaji wake,” alisema Mhe. Jamal Kassim Ali.

Aidha ameushukuru uongozi wa Wizara ya Fedha na Mipango upande wa bara kwa kikao hicho na kueleza kuwa kikao hicho ni vema kikawepo angalau kila baada ya miezi miwili ili kuona mambo mapya yatakayoibuka yanatatuliwa na kufanya ufuatiliaji wa makubaliano yaliyopita jambo ambalo lililidhiwa na pande zote.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Mawaziri Wa Fedha Tanzania Bara Na Zanzibar Kutatua Changamoto Za Miradi
Mawaziri Wa Fedha Tanzania Bara Na Zanzibar Kutatua Changamoto Za Miradi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh2a7BopOupcFaoSSQCJyRHGIOL5LgQYsYBhH3XJUVdo6z8CVyIeLPJQ6Ayh-HSu3mqW-6cgs2AOSkseFLJO2VzZP7s9xTBxaUwKNbd2OT4QOuKDQS0nKpwTvGzB1BfB1ZCPfMcpK0Vo9Qq/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh2a7BopOupcFaoSSQCJyRHGIOL5LgQYsYBhH3XJUVdo6z8CVyIeLPJQ6Ayh-HSu3mqW-6cgs2AOSkseFLJO2VzZP7s9xTBxaUwKNbd2OT4QOuKDQS0nKpwTvGzB1BfB1ZCPfMcpK0Vo9Qq/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/mawaziri-wa-fedha-tanzania-bara-na.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/mawaziri-wa-fedha-tanzania-bara-na.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy