ISHU YA USAJILI YANGA YAPEWA ONYO
HomeMichezo

ISHU YA USAJILI YANGA YAPEWA ONYO

  T AYARI Yanga  wameamua kuanza  usajili kwa ajili ya  msimu mpya wa  2021/22 ambao utakuwa  na matarajio makubwa kwa  Wanayanga.   Nas...


 TAYARI Yanga wameamua kuanza usajili kwa ajili ya msimu mpya wa 2021/22 ambao utakuwa na matarajio makubwa kwa Wanayanga.

 

Nasema Wanayanga kwa kuwa Klabu ya Yanga inaendeshwa na nguvu za wanachama na linakuwa ni jambo kubwa sana kuangalia nguvu yao wakati wanapokuwa na uhitaji.

 

Misimu minne sasa Yanga haijawahi kugusa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, jambo ambalo hata kama watakuwa hawalisemi sana lakini wanachama na mashabiki wa Yanga, litakuwa limewachosha.

 

Wanataka na wenyewe kuona timu yao inabeba ubingwa ambao unatambulika kama sehemu ya michuano sahihi inayotambulika.Tunajua, ukiachana na Ngao ya Jamii kuna ubingwa wa Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho la Azam Sports.


Yanga wamekuwa wakisuasua upande huu huku watani wao Simba wakiendelea kuchanua.Unaona, hata nafasi ya kwenda katika michuano ya kimataifa inaonekana imekuwa kwa “msaada wa Simba”, jambo ambalo kwa sasa wanaweza kuwa wanalichukulia kama mzaha lakini bila ya ubishi, watakuwa wamechoka.

 

Inawezekana kabisa uvumilivu wao sasa umefikia ukingoni na tamaa yao ni kuona Yanga inafanya vizuri na kunaweza kukawa na ugumu sana kwa kuwa matumaini makuu kwa mashabiki na wanachama wa Yanga, wamewekeza katika msimu huu ujao.

 

Msimu ujao ndio wamejaza kila kitu wakiwa na imani kubwa kwamba mambo yataamka, kwamba viongozi wao wanaelewa wanachohitaji na wanajua kabisa kwamba kuna marekebisho yatafanyika kuhakikisha wanafikia mafanikio ambayo wameyasubiri kwa wakati au muda mrefu sana.

 

Kumekuwa na maneno fulani hivi ya kuwapa matumaini, kumekuwa na maneno ambayo yamewafanya waamini kesho kuna jambo bora linakuja.

 

Ninaamini, kama Yanga itashindwa kubeba kikombe chochote kwa msimu huu ujao, hakika suala la kukata tamaa litachukua nafasi kubwa sana.Kiasili, inajulikana kuwa mashabiki wa Yanga si wavumilivu sana lakini kwa safari hii mambo yamekuwa tofauti kidogo.

 

Uvumilivu wa kipindi cha misimu minne hauwezi kuwa wa muda mfupi na lazima tutoe nafasi ya kuwapongeza mashabiki wa Yanga kwa kuwa wamejitahidi sana.

 

Angalia timu ambayo haijabeba ubingwa wa Ligi Kuu Bara kwa misimu minne lakini hawajawahi kuacha kwenda uwanjani na wamekuwa wakiendelea kuishangilia timu yao kila kukicha. Uzalendo wao hauna mfano na wanapaswa kupongezwa.

 

Wakati tunawapongeza mashabiki na wanachama wa Yanga, huu ndio wakati mwafaka wa kuwakumbusha viongozi wa Yanga tukianza na wale ambao wanahusika na usajili kwamba, makosa basi na msimu huu ni wa jambo la lazima iwe kombe au makombe.

 

Hakuna mjadala, msimu huu lazima Yanga wafanye jambo kwa kuhakikisha wanabeba kombe au makombe, la sivyo hawatakuwa na jambo au njia yoyote ya kujitetea na kutokea sehemu iliyo huru ya kusema “tumekosea tena”.

 

Simba wamejenga timu yao kwa muda mfupi na inaonekana kwa muda mfupi wamejenga kikosi chao kilichofanya vizuri kwa misimu minne mfululizo.

 

Lakini vipi Yanga kwa siku zote walizokuwa hawachukui mataji, maana yake walikuwa wanajiandaa na hata baada ya kushindwa kubeba ubingwa mara kadhaa walifanya mabadiliko.

 

Msimu mmoja kabla, walipangua karibu kikosi chote na kikosi chao kipya kikaishia nafasi ya pili nyuma ya Simba, mara mbili.

 

Sasa si wakati wa kujenga tena kikosi bila ya mafanikio na lazima hili liwe katika vichwa vya viongozi hao.Lazima tuone mafanikio ili kuonyesha kweli kuna ngazi walikuwa wanakwenda kwenye mabadiliko sahihi ya ubora.


 Hakuna ujanja, Yanga lazima wafanye vizuri hata kwa asilimia 60 kuonyesha kweli wanapiga hatua na usajili wao unapaswa kuwa usajili sahihi.

 

Yanga hawapaswi tena kubahatisha, hawapaswi tena kwenda mwendo usio na mafanikio na kama kujipanga basi kumetosha na huu

ni msimu wa kuonyesha wamejifunza kutokana na makosa na huu ni wakati wa kuonyesha ubora wao na kuangukia katika mafanikio.



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: ISHU YA USAJILI YANGA YAPEWA ONYO
ISHU YA USAJILI YANGA YAPEWA ONYO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhQ5ji6t1NpGOJuhQAiNpvJPDrAA56PldC-GwPBimDa5_Gr5Ia7w9xjNe1LC3Kf-OOB_aUC2-T5CacxoXez9jEni1CNTrlDt-ZccoqRvXQdnYbkyktfht2KL2gpgYMWqM1SaYuw7dJZVmoT/w640-h426/Makambo.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhQ5ji6t1NpGOJuhQAiNpvJPDrAA56PldC-GwPBimDa5_Gr5Ia7w9xjNe1LC3Kf-OOB_aUC2-T5CacxoXez9jEni1CNTrlDt-ZccoqRvXQdnYbkyktfht2KL2gpgYMWqM1SaYuw7dJZVmoT/s72-w640-c-h426/Makambo.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/ishu-ya-usajili-yanga-yapewa-onyo.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/ishu-ya-usajili-yanga-yapewa-onyo.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy