DIDIER GOMES ANA OFA NNE MKONONI, HATMA YAKE SIMBA IPO HIVI
HomeMichezo

DIDIER GOMES ANA OFA NNE MKONONI, HATMA YAKE SIMBA IPO HIVI

 IMEELEZWA kuwa Kocha Mkuu wa Simba, Didier Gomes ana ofa nne mkononi kutoka kwa timu tofauti ambazo zinahitaji kupata saini yake. Sababu...


 IMEELEZWA kuwa Kocha Mkuu wa Simba, Didier Gomes ana ofa nne mkononi kutoka kwa timu tofauti ambazo zinahitaji kupata saini yake.

Sababu kubwa ya Gomes kuwa kwenye rada katika timu tofauti ni ubora wake ambao ameweza kuonyesha akiwa na kikosi hicho ikiwa ni msimu wake wa kwanza baada ya kurithi mikoba ya Sven Vandenbroeck.

Miongoni mwa timu ambazo zinahitaji saini yake ni pamoja na Raja Casablanca ya Morocco, Mamelod Sundowns pamoja na timu nyingine kutoka Misri.

Kwa sasa Gomes yupo zake nchini Ufaransa kwa ajili ya mapumziko baada ya ligi kuisha na ni Septemba 25 mechi ya ufunguzi ya Ngao ya Jamii inatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa ambapo itakuwa ni Simba v Yanga.

Habari zimeeleza kuwa kabla ya kusepa Bongo alikutana na Mohamed Dewji ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya  Wakurugenzi ndani ya Simba.

"Kabla ya Gomes kusepa Bongo alikutana na Mo na kufanya naye mazungumzo, walizungumza pia kuhusu mkataba wake ambapo aliweka wazi kwamba alikuwa na ofa kutoka timu mbalimbali.

"Kutokana na utendaji wake kazi mzuri walikubaliana kumuongezea mkataba hivyo bado yupo kwa kuwa alisaini dili la mwaka mmoja," ilieleza taarifa hiyo.

Julai 30, Mo aliongea na Waandishi wa Habari katika Ukumbi uliopo ndani ya Hotel ya Golden Jubilee na aliweka wazi kwamba amekuwa akitumia gharama kubwa kwa ajili ya usajili wa Simba ikiwa ni pamoja na kuwaleta makocha na yote hayo yanatokana na mapenzi ya timu hiyo tangu akiwa mdogo.




Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: DIDIER GOMES ANA OFA NNE MKONONI, HATMA YAKE SIMBA IPO HIVI
DIDIER GOMES ANA OFA NNE MKONONI, HATMA YAKE SIMBA IPO HIVI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiA3BQZ3QbpJHL4kBlE4S6ySKezUk7I_edOBitib5NFj0eHeefJQKUgSidFmRqZg1NZL9R0M3HvFDTyL0uJCh0BPzQMGTsIj4BNKPWwhqq_HHba_h12hGtqfmSZqkz97DDBZRq-FVDC0pkl/w512-h640/simbasctanzania-232144127_402345018082077_27796031721440613_n.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiA3BQZ3QbpJHL4kBlE4S6ySKezUk7I_edOBitib5NFj0eHeefJQKUgSidFmRqZg1NZL9R0M3HvFDTyL0uJCh0BPzQMGTsIj4BNKPWwhqq_HHba_h12hGtqfmSZqkz97DDBZRq-FVDC0pkl/s72-w512-c-h640/simbasctanzania-232144127_402345018082077_27796031721440613_n.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/didier-gomes-ana-ofa-nne-mkononi-hatma.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/didier-gomes-ana-ofa-nne-mkononi-hatma.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy