Naibu Waziri Mabula Apiga Marufuku Wanaoshitakiana Mabaraza Ya Ardhi Kugharamia Usafiri
HomeHabari

Naibu Waziri Mabula Apiga Marufuku Wanaoshitakiana Mabaraza Ya Ardhi Kugharamia Usafiri

Na Munir Shemweta, SONGWE Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amepiga marufuku wananchi wanaoshitakiana kwenye Mabaraza ...

Samia Suluhu Hassan aapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
LIVE: Mama Samia Suluhu anaapishwa kuwa Rais wa Tanzania
Makamu Wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan Kuapishwa Leo


Na Munir Shemweta, SONGWE
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amepiga marufuku wananchi wanaoshitakiana kwenye Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya wilaya kugharamia usafiri wa kwenda uwandani wakati wa kusikiliza mashauri ya ardhi.

Akizungumza wakati wa kuzindua Baraza la Ardhi na Nyumba la wilaya, mkoa wa Songwe jana  Dkt Mabula alisema, asingependa kuona wananchi  wanaoshitakiana katika kesi ya ardhi mmoja wao atoe fadhila ya usafiri wa kwenda uwandani.

‘Tusingependa wale wanaoshitakiana mmoja wao atoe fadhila ya usafiri maana baada ya hapo mara nyingi wazee wa Baraza wanashawishika na kuona anayetoa usafiri kuwa amekuwa ni msamamaria mwema kwa hiyo wanamlipa fadhila hata kama hana haki ya kupata ushindi’ alisema Naibu Waziri Mabula.

Aliwataka Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi kuandaa ratiba za mashauri ya Ardhi kwenye maeneo yao na kuzipeleka kwa wakuu wa wilaya aliowaeleza kuwa watashirikiana na wakurugenzi wa halmashauri kuangalia ratiba na kutoa usafiri kwa wazee wa mabarza   ili kwenda uwandani wakati wa mashauri.

Naye Kamishna wa Ardhi Nchini Methew Nhonge alisema pamoja na kuwa sheria ya ardhi imeanisha utaratibu mzuri wa kisheria katika kushughulikia migogoro ya ardhi lakini halmashauri na ofisi za ardhi za mikoa zinao wajibu mkubwa wa kuhakikisha migogoro ya ardhi kabla haijaenda mahakamani inatatuliwa kwa njia ya kiutawala.

‘Bahati nzuri katika wizara tumeweka utaratibu kwa nchi nzima kuhakikisha kwamba viongozi wa ardhi wa mkoa pamoja na halmashauri kupitia watendaji wa sekta wanaenda kwenye ngazi za halmashauri na mitaa kutoa elimu na kushughulikia migogoro ya wananchi kiutawala’’ alisema Nhonge.

 Kwa upande wake Msajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya wilaya nchini Stela Tullo aliushurukuru uongozi wa mkoa wa Songwe kwa kusaidia kupata jengo la Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya na kueleza kwamba, uanzishwaji baraza hilo utasaidia kuondoa usumbufu waliokuwa wakiupata wananchi wa Songwe kusafiri  umbali mrefu kufuata huduma za Baraza mkoani  Mbeya.

‘Ninawasihi wananchi wa Songwe kulitumia vizuri baraza la ardhi la mkoa wa Songwe kupata huduma, ile migogoro ya ardhi iliyoshindwa kusuluhishana nyumbani hata katika ngazi ya familia na mabaraza ya ardhi ya vijiji na kata basi serikali imewasogezea huduma kwenye baraza la ardhi na nyumba la wilaya  mkoa wa Songwe’’ alisema Stela Tullo.

Kabla ya uzinduzi wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya, mkoa wa Songwe, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula alizindua Baraza kama hilo  wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya ambapo aliagiza mashauri ya ardhi yasikilizwe na kuisha katika kipindi kisichozidi miaka miwili.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Naibu Waziri Mabula Apiga Marufuku Wanaoshitakiana Mabaraza Ya Ardhi Kugharamia Usafiri
Naibu Waziri Mabula Apiga Marufuku Wanaoshitakiana Mabaraza Ya Ardhi Kugharamia Usafiri
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgJ3kq9PfFvwe_z-af1Y7ZUfBw1tUD5f0aAp1q-ypBRg8cWQeYv603Qfh4eBPrfdmh_LNkrPSN9oNKT90wJt22qCZ6Jd29uCn707LV10n-hxPFss3wXUovNTLey6Cyr-aTmer0hMf0Rm1jq/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgJ3kq9PfFvwe_z-af1Y7ZUfBw1tUD5f0aAp1q-ypBRg8cWQeYv603Qfh4eBPrfdmh_LNkrPSN9oNKT90wJt22qCZ6Jd29uCn707LV10n-hxPFss3wXUovNTLey6Cyr-aTmer0hMf0Rm1jq/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/07/naibu-waziri-mabula-apiga-marufuku.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/07/naibu-waziri-mabula-apiga-marufuku.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy