Majaliwa: Wizara Ya Kilimo Hakikisheni Ushirika Unakuwa Endelevu
HomeHabari

Majaliwa: Wizara Ya Kilimo Hakikisheni Ushirika Unakuwa Endelevu

Waziri Mkuu ameiagiza Wizara ya Kilimo isimamie kikamilifu changamoto mbalimbali zinazodumaza vyama vya ushirika nchini ili kujenga ushi...


Waziri Mkuu ameiagiza Wizara ya Kilimo isimamie kikamilifu changamoto mbalimbali zinazodumaza vyama vya ushirika nchini ili kujenga ushirika imara unaokuwa na endelevu.

Pia, Mheshimiwa Majaliwa ameiagiza wizara hiyo ihakikishe inavijengea vyama vya ushirika uwezo wa kujiendesha kiushindani na kuimarisha utafutaji wa masoko ya ndani na nje.

Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo jana (Jumamosi, Julai 3, 2021) kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika Kitaifa katika viwanja vya lipuli, Tabora.

Amesema ushirika ni chombo ambacho kinajenga imani kwa wakulima na wanaushirika na kwa kuwa Serikali inaweka nguvu katika jambo hilo kwa lengo la kuona ushirika unaleta manufaa.

“Natambua kuwa ushirika ndicho chombo madhubuti cha kuwauunganisha wakulima, wafugaji na wavuvi na kuwapa uwezo na nguvu ya kutatua matatizo yao ya kiuchumi na kijamii.”

Amesema wizara hiyo inatakiwa iimarishe usimamizi na udhibiti wa vyama hivyo sambamba na kuviwezesha kusimamia mifumo rasmi ya masoko ukiwemo wa Stakabadhi ghalani.

Amesema utoaji wa elimu na mafunzo ya ushirika kwa wanachama, viongozi na watendaji ni vema ukaimarishwa ili waweze kuelewa vizuri dhana ya ushirika, misingi, kanuni na taratibu.

Kadhalika, Waziri Mkuu ameliagiza Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) libadilishe mfumo wa ukaguzi na lihakikishe linatoa taarifa sahihi kwa wakulima.

Waziri Mkuu amesema katika mwaka wa fedha 2020/2021, Serikali kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika imefanya ukaguzi wa ndani wa vyama vya ushirika 4,494 kati ya 9,185.

Pia, Waziri Mkuu amewataka Warajisi wote wahakikishe kila ushirika katika maeneo yao unakuwa na kanzi data za wanaushirika wote. “Lazima uwe na takwimu za wanaushirika wote.”

Amesema lengo la kuwa na takwimu hizo ni kuweza kufanya makadirio ya kupeleka mahitaji mbalimbali kwa wakulima ikiwa ni pamoja na mbegu, mbolea na dawa za kuulia wadudu.

Kwa upande wake, Waziri wa Kilimo, Prof. Adolf Mkenda ametumia fursa hiyo kumpongeza Mheshimiwa Majaliwa kwa jitihada zake za kufufua na kuendeleza vyama vya ushirika nchini.

“Wewe binafsi Mh. Waziri Mkuu umesimamia shughuliza ushirika kwa moyo mmoja. Umetusaidia kurudisha mali za vyama vya ushirika ambazo zilitoka kinyume na utaratibu.”

“Kwa juhudi hizi Mhe. Waziri Mkuu umetusaidia sana kurudisha imani kwa wana-ushirika kwamba wakiwa kwenye ushirika mali zao haziwezi kufanyiwa ubadhilifu wa aina yoyote.”

Waziri huyo ametaja vyama ambavyo Mheshimiwa Waziri Mkuu alisimamia urejeshwaji wa mali zake kuwa ni pamoja na mali za NCU-Mwanza, SHIRECU-Shinyanga, KNCU, KCU.

Pia, Waziri huyo amemuahidi Waziri Mkuu kwamba wataendelea kusimamia ushirika nchini na kuhakikisha unaendeshwa kwa weledi, uwajibikaji na uwazi ili watu wengi wapende kujiunga.

(Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Majaliwa: Wizara Ya Kilimo Hakikisheni Ushirika Unakuwa Endelevu
Majaliwa: Wizara Ya Kilimo Hakikisheni Ushirika Unakuwa Endelevu
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiReTWnspqfYx5UGD8ZiI2nitHNQJHNpiTfcQHwARFersJ_opSEWpWizIxIC26Pr63DKgMixwclN-zxiKdgDsBhEMYcJFXX9yo9KZsL2ZDjltovxrBp4JMjk2D8aXD90aV4Md9veTQ13BLb/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiReTWnspqfYx5UGD8ZiI2nitHNQJHNpiTfcQHwARFersJ_opSEWpWizIxIC26Pr63DKgMixwclN-zxiKdgDsBhEMYcJFXX9yo9KZsL2ZDjltovxrBp4JMjk2D8aXD90aV4Md9veTQ13BLb/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/07/majaliwa-wizara-ya-kilimo-hakikisheni.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/07/majaliwa-wizara-ya-kilimo-hakikisheni.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy