Hospitali ya Maswa Yapinga habari za uhaba wa dawa.
HomeHabari

Hospitali ya Maswa Yapinga habari za uhaba wa dawa.

Samirah Yusuph. Maswa. Kufuatia tetesi zilizosambaa katika mitandao ya kijamii kuhusu kukosekana kwa dawa hata "Panadol"  kat...

Habari kubwa Magazetini Kenya leo October 31, 2024
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo October 31, 2024
Miradi 77 inaendelea kutekelezwa na Tanroads nchini


Samirah Yusuph.
Maswa.
Kufuatia tetesi zilizosambaa katika mitandao ya kijamii kuhusu kukosekana kwa dawa hata "Panadol"  katika hospitali ya wilaya ya Maswa, mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Fredrick Sagamiko amesema taarifa hiyo sio sahihi.

Sagamiko amesema kuwa hali ya upatikanaji wa madawa katika hospital ya wilaya hiyo ni asilimia 98 na upatikanaji wa madawa muhimu ni 100 na kuwa halmashauri hiyo inaduka la madawa bora miongoni mwa maduka yote ya madawa nchini.

"Taarifa hiyo haina ukweli, kuna dawa za kutosha na duka la dawa linalo milikiwa na hospital ya wilaya ya Maswa ndilo duka linalouza dawa katika zahanati, vituo vya afya na hospitali zote za Mkoa wa Simiyu pia tuna mfumo wa "hospital protocol" unaowezesha ofisi ya mkoa kupata taarifa za utoaji wa dawa kwa kila wiki kwa hospitali zote"

Ameongeza kuwa hapo mfumo wa utoaji taarifa za dawa katika ofisi ya mkuu wa wilaya imesaidia kuondoa kwa kiasi kikubwa upotevu wa dawa katika vituo vya kutolea huduma za afya hivyo dawa stahiki zinawafikia wahitaji bila kuwa na shaka.

Aidha kwa upande wake mganga mfawidhi wa hospitali hiyo James Bwire alisema kuwa mahitaji ya dawa katika hospitali hiyo yanajitosheleza na kuwa hospitali hiyo inamaduka matatu ya dawa ambalo ni duka la wateja wa bima, duka linalo hudumia zahanati, vituo vya afya na hospitali nyingine pamoja na duka la hospital.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi Diwani wa kata ya Binza Aroni Joseph Mboje alisema kuwa shida na madawa ilikuwepo kipindi cha nyuma lakini kwa sasa haipo tena mambo yanayo jitokeza katika mikutano sio uhalisia kwa sasa dawa zipo za kutosha.

"Vitu wanavyovisema wananchi hawana uhakika navyo baada ya taarifa hiyo nilifika hospitali kuja kujionea lakini kuna dawa nyingine wanaandikiwa wakachukue maduka ya nje hivyo wanasema hospitali haina dawa lakini dawa zipo za kutosha".

 Mwisho.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Hospitali ya Maswa Yapinga habari za uhaba wa dawa.
Hospitali ya Maswa Yapinga habari za uhaba wa dawa.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjvGw9qcxL8247fxI7-AkvBzorKC22chj4le6WtvWRkYyH6PA7hUtf7CHDzt6iIFKkXqJ8tbRuVbq37ZXB4SRuoIY7DrFc7Xd90nxq4kxy4hh5pUQ8uljxZeltv6mW0XwAZa3XhyphenhyphenZ8rQ-CN/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjvGw9qcxL8247fxI7-AkvBzorKC22chj4le6WtvWRkYyH6PA7hUtf7CHDzt6iIFKkXqJ8tbRuVbq37ZXB4SRuoIY7DrFc7Xd90nxq4kxy4hh5pUQ8uljxZeltv6mW0XwAZa3XhyphenhyphenZ8rQ-CN/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/07/hospitali-ya-maswa-yapinga-habari-za.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/07/hospitali-ya-maswa-yapinga-habari-za.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy