Waziri Mkenda Aanza Mkakati Kupunguza Bei Ya Mbolea
HomeHabari

Waziri Mkenda Aanza Mkakati Kupunguza Bei Ya Mbolea

 Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma Serikali imeielekeza Mamlaka ya Mbolea Tanzania (TFRA) kuanza kutoa vibali vya kuuza mbolea a...


 Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Serikali imeielekeza Mamlaka ya Mbolea Tanzania (TFRA) kuanza kutoa vibali vya kuuza mbolea ambayo imeshaingia nchini (Export Permit) badala ya vibali hivyo kutolewa ofisi ya Waziri wa Kilimo.

Waziri wa Kilimo Mhe Prof Adolf Mkenda ametoa maelekezo hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mara baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Muwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Mbolea (YARA) Ofisini kwake Jijini Dodoma

Ili kuongeza ufanisi zaidi wa utendaji Waziri Mkenda amesema kuwa vibali hivyo vitatolewa kwa njia ya mtandao (Online) badala yake Ofisi ya Waziri wa Kilimo itakuwa na jukumu la kupewa taarifa ya utekelezaji wa utoaji vibali uliofanywa na TFRA.

Waziri Mkenda amesema kuwa serikali ina matumaini makubwa na wafanyabiashara wa mbolea kwani inaamini kuwa kurahisishwa utolewaji wa vibali hivyo kutawaongezea kasi ya kuagiza mbolea nyingi itakayoingia nchini kwa ajili ya matumizi ya wakulima wa ndani na nje ya nchi.

Amesema kuwa kufuatia uingizwaji mwingi wa mbolea nchini jambo hilo litaimarisha uwezekano wa upatikanaji wa mbolea kwa bei nafuu kwa wakulima jambo litakalopelekea kuongezeka tija na uzalishaji kwa wakulima.

Kuhusu gharama za usafirishaji wa mbolea kupitia barabara, Waziri Mkenda amesema kuwa atafanya mazungumzo na Hazina ili kuona uwezekano wa huduma za kusafirisha mbolea kama itawezekana kutoa VAT.

“Tumegundua kuwa kusafirisha mbolea kwa reli kunapunguza sana gharama kwahiyo tumehimiza mbolea isafirishwe kwa reli kwenda kaskazini kwa maana ya mikoa ya Kilimanjaro, Tanga, Arusha na Manyara pamoja na kusafirishwa kwa reli kupitia njia ya kati mikoa ya Morogoro, Singida, Dodoma, Singida N.k na Tazara tutafanya hivyo” Amekaririwa Prof Mkenda

Waziri Mkenda amesema kuwa ili kupunguza gharama za mbolea nchini serikali imeielekeza Mamlaka ya Mbolea TFRA kuhakikisha kuwa inaongeza muda wa zabuni ambao walikuwa wameutoa.

Kuhusu Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC), Waziri Mkenda amesema kuwa katika makubaliano ya kikao kazi cha wizara atatafutwa mtaalamu elekezi  kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam shule ya Biashara kukaa kwa kipindi cha miezi sita na kuishauri serikali nini kifanyike ili kuifufua taasisi hiyo.

Naye Mkurugenzi wa Maendeleo ya Mazao Wizara ya Kilimo Ndg Nyasebwa Chimagu amesema kuwa Waziri wa Kilimo ameendelea kukutana na wadau wa mbolea nchini ili kuhakishisha kuwa wakulima wanaendelea kuzalisha kwa wingi mazao ya chakula na biashara hivyo ili kufikia hatua hiyo ni lazima kuongeza matumizi sahihi ya mbolea kwa wakulima.

Amesema kuwa nchi mbalimbali duniani zinaitegemea bandari ya Dar es salam katika kusafirisha mbolea hivyo vibali vya usafirishaji wa mbolea kutolewa moja kwa moja na TFRA itaongeza chachu ya urahisishaji kwa wauzaji wa mbolea lakini pia kurahisisha upatikanaji wa mbolea kwa haraka.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri Mkenda Aanza Mkakati Kupunguza Bei Ya Mbolea
Waziri Mkenda Aanza Mkakati Kupunguza Bei Ya Mbolea
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgikfiarvJzYNPc1Q5Y8mdJWICtBjd6AN7XOA_Gd93XHH4YATBrV5to9Qck5493kJtPuu0bglyWN88F0Niutf3O6qn0f4_WBG_rH-8uCkcLuT1kHU7-RRbMiqTO6VbnWdaBsiXtPa2woyHX/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgikfiarvJzYNPc1Q5Y8mdJWICtBjd6AN7XOA_Gd93XHH4YATBrV5to9Qck5493kJtPuu0bglyWN88F0Niutf3O6qn0f4_WBG_rH-8uCkcLuT1kHU7-RRbMiqTO6VbnWdaBsiXtPa2woyHX/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/waziri-mkenda-aanza-mkakati-kupunguza.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/waziri-mkenda-aanza-mkakati-kupunguza.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy