UCHAGUZI 2021...TFF KIMYAKIMYA WATINGA FIFA, WAZUA HOFU
HomeMichezo

UCHAGUZI 2021...TFF KIMYAKIMYA WATINGA FIFA, WAZUA HOFU

Na Mwandishi Wetu SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limefanya mawasiliano na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) kuhusiana na uchaguz...

MCHEZO WA KIMATAIFA DHIDI YA AL MERRIKH WAMFIKIRISHA GOMES
YANGA KUPELEKWA FIFA NA SIBOMANA,KISA MKWANJA
MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA SPOTI XTRA JUMAPILI

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limefanya mawasiliano na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) kuhusiana na uchaguzi mkuu wa shirikisho hilo uliopangwa kufanyika Agosti 7 mjini Tanga.

Imeelezwa, TFF imeishitakia Fifa kuhusiana na baadhi ya wabunge kuishawishi Serikali kuingilia uchaguzi huo ambao uko katika hatua za awali kabisa.

Taarifa za ndani kutoka katika shirikisho hilo, zimeeleza kumekuwa na mawasiliano kati ya TFF na Fifa kuhusiana na uchaguzi huo, hata hivyo haikuelezwa awali TFF wameieleza nini Fifa.

Mara nyingi, Fifa wamekuwa wakitoa adhabu ya kuzifungia nchi ambazo Serikali zake zimekuwa zikiingilia uchaguzi wa mashirikisho, hali ambayo baadhi ya wadau wameieleza kuwa kama ni tatizo kama wabunge wataendelea kuitaka Serikali iingilie uchaguzi huo.

Juhudi za kuwapata viongozi wa TFF jana zilishindikana kutaka kujua nini hasa ambacho TFF wamekuwa wakiwasiliana na Fifa kuhusiana na uchaguzi huo ambao umepamba moto.

Juzi na jana, baadhi ya waliotaka kugombea akiwemo Mbunge wa Mwelra, Zahoro Mohamed Haji walilalamika kushindwa kupata ruhusa ya kugombea kutoka kwa wanachama wa shirikisho hilo.

 Kila mgombea hutakiwa kupata kura angalau tano kutoka kwa wanachama zaidi ya 40 wa shirkisho hilo.

Imeonekana Rais wa TFF, Wallace Karia na mgombea mwingine aitwaye, Evance Mguesa ndio waliofanikiwa kupata kuaminiwa na wanachama hao, jambo ambalo limelalamikiwa na wagombea hao huku wengine wakilalamika kuitaka Serikali iingilie uchaguzi huo wa TFF.


Leo asubuhi juhudi za kumpata Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidao zilifanikiwa na akasema wamekuwa na mawasiliano na Fifa si kwa ajili ya kushitaki na badala yake ni utaratibu wa kawaida.

“Ni utaratibu wa kawaida kabisa kuwasiliana na Fifa kwa ajili ya kuwaeleza mchakato wa uchaguzi unakwenda vipi. Tunawaeleza mambo yote, kwamba kuna malalamiko, jambo ni hili na kadhalika,” alisema Kidao.

Kidao alisema wao hawana sababu ya kuichongea Serikali kwa kuwa wanaporipoti Fifa lazima wafanye hivyo kwa Serikali pia kwa kuwa inapaswa kujua mchakato wa uchaguzi unaendeleaje pia.


“Serikalini pia tunaripoti kama tunavyofanya kwa Fifa, lazima Serikali ijue nini kinaendelea na uchaguzi umefikia wapi. Huu ni wajibu wetu kufanya hivi kwa Serikali na Fifa.”




Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: UCHAGUZI 2021...TFF KIMYAKIMYA WATINGA FIFA, WAZUA HOFU
UCHAGUZI 2021...TFF KIMYAKIMYA WATINGA FIFA, WAZUA HOFU
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgs2SaZa6un_a4T0Y_35hnopbYCsa6dxkCVVryZp-2jdMVYL2kzd8tDT9YlLAReIg5kLzwMVcGOqUJPRo90lTW6DK6rGSqvrVMlFCVZmuW8MfEKXERpdhNtfVAdV-pOdL0tdztKl03OfbLh/w640-h360/Fifa.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgs2SaZa6un_a4T0Y_35hnopbYCsa6dxkCVVryZp-2jdMVYL2kzd8tDT9YlLAReIg5kLzwMVcGOqUJPRo90lTW6DK6rGSqvrVMlFCVZmuW8MfEKXERpdhNtfVAdV-pOdL0tdztKl03OfbLh/s72-w640-c-h360/Fifa.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/uchaguzi-2021tff-kimyakimya-watinga.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/uchaguzi-2021tff-kimyakimya-watinga.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy