Mradi Bandari ya Bagamoyo kufufuliwa
HomeHabari

Mradi Bandari ya Bagamoyo kufufuliwa

Rais Samia Suluhu Hassan amesema Serikali imeamua kufufua mazungumzo ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo na mradi w...


Rais Samia Suluhu Hassan amesema Serikali imeamua kufufua mazungumzo ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo na mradi wa Mchuchuma na Liganga ili kuchochea kasi ya kukuza uchumi nchini.

Alisema hayo jana Dar es Salaam alipofungua Mkutano wa 12 wa Sekretarieti ya Baraza la Taifa la Biashara (TBNC)  uliohudhuriwa na wajumbe 50  ambao 25 sekta binafsi na  wengine sekta ya umma. Ulishirikisha pia wawakilishi wa wafanyabiashara kutoka mikoani, mashirika ya kimataifa na wawekezaji.

Alisema ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo ni muhimu kwa sababu utaongeza uwezo wa kushindana na bandari shindani na kukuza uchumi wa Taifa.


Kuhusu mikakati ya kuzisaidia sekta za utalii na usafiri wa anga ambazo zimeathiriwa na ugonjwa wa corona, Rais Samia amesema Serikali imepunguza ada mbalimbali ikiwa ni pamoja na ada ya Wakala wa Wasafirisha Watalii kutoka Dola za Marekani 2,000 hadi Dola 500 kwa kampuni yenye magari kati ya 1 na 3.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Sekta binafisi nchini (TPSF), Angelina Ngalula ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kujenga mazingira bora na rafiki kwa Wafanyabiashara na Wawekezaji kutokana na hatua mbalimbali zinazochukuliwa ikiwa ni pamoja na kufuta baadhi ya kodi na tozo ambazo zimesaidia kuimarisha biashara na uwekezaji nchini.

Baraza la Biashara la Taifa (TNBC) limeanzishwa likiwa ni jukwaa rasmi la majadiliano kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi ili kuwezesha kupatikana kwa muafaka wa pamoja kuhusu masuala muhimu yanayohusu maboresho ya Sera, Sheria, Kanuni na Taratibu za biashara na uwekezaji nchini.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Mradi Bandari ya Bagamoyo kufufuliwa
Mradi Bandari ya Bagamoyo kufufuliwa
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhXQXuLU_4CpOwNDJ8S4vQiFUFggtHBrKYDehnCevHCDHn_hg0CMbIamjn9glAaJCg7gyEyhnYeJLTUPDY-TcPlocX7TNJxp7rS2_iwWAgypZ-tI50u-26l5uDiPWDEMHY-XU2RvOYJSp34/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhXQXuLU_4CpOwNDJ8S4vQiFUFggtHBrKYDehnCevHCDHn_hg0CMbIamjn9glAaJCg7gyEyhnYeJLTUPDY-TcPlocX7TNJxp7rS2_iwWAgypZ-tI50u-26l5uDiPWDEMHY-XU2RvOYJSp34/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/mradi-bandari-ya-bagamoyo-kufufuliwa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/mradi-bandari-ya-bagamoyo-kufufuliwa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy